• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:25 PM
Magoha kuongoza kikao kuhusu mitihani

Magoha kuongoza kikao kuhusu mitihani

Na CECIL ODONGO

WAZIRI wa Elimu, Prof George Magoha leo Jumatatu anatarajiwa kukutana na wadau katika sekta ya elimu kupanga namna ya kuendesha mitihani ya kitaifa ya KCPE na KCSE inayonukia, mkutano utakaofanyika katika Kenya School of Government eneo la Kabete.

Prof Magoha anatarajiwa kukutana na Washirikishi wa elimu kutoka maeneo yote nchini pamoja na wakurugenzi wa elimu katika kaunti na kaunti-ndogo kote nchini.

KCPE inatarajiwa kuanza Oktoba 28 hadi Oktoba 31 huku KCSE ikianza Novemba 4 hadi Novemba 27.

Wanafunzi 1,089,671 wanatarajiwa kufanya mtihani wa KCPE huku wengine 698,935 wakifanya mtihani wa KCSE.

Baadhi ya mambo yanayotarajiwa kujadiliwa ni namna mitihani hiyo itakavyosafirishwa, usalama wa karatasi za mitihani na namna ya kuzuia visa vya udanganyifu.

Aidha, waziri huyo amekuwa akitoa onyo kali kwa walimu wakuu wanaoshirikiana na baadhi ya watu kisha kuwahadaa wanafunzi kuchangisha fedha kununua mitihani hiyo kwamba wataadhibiwa vikali.

You can share this post!

Madeni sasa yamelemea nchi – Sapit

Oparanya ashutumu wanaopinga juhudi za kufufua Mumias Sugar

adminleo