• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Trump atarajiwa kuzuru Kenya

Trump atarajiwa kuzuru Kenya

Na PRAVINDOH NJUGUNATH

RAIS wa Amerika Donald Trump anatarajiwa kuzuru Kenya wiki ijayo katika ziara yake ya kwanza barani Afrika.

Trump anapaniwa kuzindua barabara Kuu ya Mombasa- Nairobi inayoendelea kupanuliwa kwa ufadhili kutoka serikali yake na ile ya Kenya.

Serikali ya Kenya imekaa kimya kuhusu ziara hiyo ya siku tatu ya Rais Trump kwa sababu ya usalama wa kiongozi huyo wa taifa lenye uwezo zaidi duniani.

Uchunguzi wa Taifa Jumapili umebainisha kuwa tayari maafisa wa Federal Bureau of Investigation (FBI) kutoka Amerika wamewasili nchini na wanaendelea kushirikiana na wenzao wa Kenya kulainisha usalama wa Trump.

“Tayari tumepokea zaidi ya maafisa 100 wa FBI na tumewatuma maeneo ambayo Trump atatembelea wakati wa ziara yake,” alisema Mkuu wa Polisi jijini Nairobi Seetanoh Lutchmeenaraidoh.

Bw Lutchmeenaraidoh hata hivyo, hangethibitisha iwapo maafisa hao wa FBI wamekuja kwa sababu ya ziara hio ya Trump, lakini alisema Kenya inatarajia ‘mgeni mashuhuri.’

Duru ziliambia Taifa Jumapili kuwa kutimuliwa kwa Balozi wa Amerika humu nchini Robert Godec kulikuwa sehemu ya kutayarisha ziara ya Trump,kwa kuleta balozi mwingine ‘anayekubalika’ na Wakenya wote.

Hivi majuzi, aliyekuwa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Amerika Rex Tillerson alifika nchini kwa kile kilionekana kama kuandaa ziara ya kiongozi huyo.

Barabara Kuu ya Mombasa- Nairobi imepanuliwa kwa gharama ya Sh380 bilioni na kiasi kikubwa cha fedha hizo kimefadhiliwa na serikali ya Trump.

 

You can share this post!

‘Ni kibarua kigumu kumsaidia Miguna’

Mhubiri agunduliwa mkulima wa bangi shambani mwake

adminleo