• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Tamasha zang’oa nanga kwa shairi la kusisimua

Tamasha zang’oa nanga kwa shairi la kusisimua

Na ANTHONY NJAGI

AWAMU ya 59 ya michezo ya kuigiza ya kitaifa baina ya shule na vyuo yalianza Jumanne katika shule ya wavulana ya Lenana, Kaunti ya Nairobi.

Shule ya Laiser Hill Academy ilikuwa ya kwanza jukwaani katika tamasha hizo ziliizofunguliwa rasmi na Kamishna wa eneo la Nairobi, Bw Kang’ethe Thuku.

Mwanafunzi Lennox Agwenge wa Laiser Hill Academy kutoka Rift Valley aliwasilisha shairi la kuigizwa lenye kichwa “The Hotbed” ambalo linatoa hadithi kuhusu shule katika kijiji maskini ambayo inashiriki mashindano hayo ya kuigiza kwa mara ya kwanza.

Wanafunzi hao wanaonekana kushtuliwa sana na jinsi shule nyingine zimewekeza katika mavazi na ala nyingine za kutumia jukwaani. Kutokana na hali hiyo, washiriki wanajawa na wasiwasi ikiwa wao kweli watafaulu ama kupitisha ujumbe wao.

Lakini mambo yanaenda kinyume na matarajio yao, baada ya kuhitimu kuendelea kwa kuwa ujumbe wao ulionekana kufaa.

Shairi hilo limeandikwa na Clifford Ouma al maarufu Nyakwar Dani, na linasheheni vichekesho tele.

Mwandishi huyo amewahi kushirikiana na Shule ya Sekondari ya Highway hata kwa shairi maarufu la Otonglo Time lililowasilishwa na Daniel Owira, mnamo 2010, na ambaye alidhaminiwa na Rais Uhuru Kenyatta kwa masomo yake, baada ya kushiriki tamasha hizo.

Shule ya Upili ya Kenya High ilikuwa na densi ya “Alando”. Densi hiyo inamzungumzia msichana kwa jina Alando ambaye anatelekezwa na wazazi wake ambao wamejali zaidi taaluma zao na kumwachia mjakazi “jakasi” jukumu la ulezi.

Jakasi ni mcha Mungu na mwenye kuamini sana maombi, na anaonekena akimuombea sana Alando. Lakini wazazi wanaishia kumshtumu kwa kujaribu kumbadilisha mtoto wao dini.

Jambo hilo, linamkasirisha Alando ambaye anaamua “kumwaga mtama” kuhusu wazazi wake ambao wamemsahau na anaelezea kuwa anayemlea ni Jakasi.

Densi hiyo inaongozwa na Janice Njuguna, Sumeiya Salim, Kellen Amimo, Brenda Ouma na ilitayarishwa na Henry Wanjala.

Shule ya Upili ya Menengai kutoka Rift Valley  ilikuwa na mchezo “Gorias Glory’’ ulioandikwa na Michael Kiguta. Mchezo huo unaelezea jinsi wavulana na wasichana wamewachwa kujitafutia maisha bila mwelekeo wowote.

“Kwa kipindi cha miaka mitano, tumekuwa kwa mashindano ya kitaifa na siri ni kushirikiana na wanafunzi kuanzia wakati wa kutayarisha hadithi hadi inapokamilika kutayarishwa,” alieleza Bw Kiguta.

Tamasha hizo pia zinashuhudia jinsi wazazi wanafaa kuzingatia talanta na sio masomo pekee.

 

You can share this post!

Ruto ndiye suluhu tosha ya tatizo la ardhi Pwani, asema...

FUNGUKA: Ole wenu mnaoingia mtegoni…

adminleo