• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 1:47 PM
Wafanyakazi wa Tuskys watisha kugoma

Wafanyakazi wa Tuskys watisha kugoma

Na BERNARDINE MUTANU

Wafanyikazi wa Tuskys wanalenga kugoma katika muda wa wiki mbili zijazo kwa kulalamika kufanyiwa hila na mwajiri wao.

Walitoa notisi ya kwenda mgomo Jumanne kupitia kwa chama chao cha wafanyikazi. Wafanyikazi hao walilalamika kuhamishwa kwa wasimamizi wengi wa wafanyikazi wa maduka hayo na kukosa kwa mwajiri wao kuwatambua wasimamizi hao kama wawakilishi wao.

Miongoni mwa malalamishi yao ni kuhusiana na kukosa kwa kampuni hiyo kutii maagizo ya mahakama kuhusu huduma za kutoka nje na hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi ya wasimamizi wao.

Kulingana na katibu mkuu wa chama hicho Boniface Kavuvi, juhudi za kusuluhisha mzozo huo kwa njia ya mazungumzo zimegonga mwamba, hivyo, baada ya wiki mbili ikiwa malalamishi yao hayatakuwa yamesikilizwa na kusuluhishwa wataenda mgomo.

You can share this post!

Mfanyabiashara aitaka bunge limtimue Matiang’i kazini

Msako dhidi ya Al-Shabaab msituni Boni waanzishwa

adminleo