• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Shujaa yalemewa na Fiji kwenye fainali

Shujaa yalemewa na Fiji kwenye fainali

Na CHRIS ADUNGO

TIMU ya Kenya ya raga ya wachezaji saba kila upande, Shujaa, Jumapili ilipata kadi mbili za manjano katika kipindi cha kwanza na kuzima matumaini ya kutwaa ubingwa wa Hong Kong Sevens, baada ya fiji kuipiga 24-12 na kuetetea ubingwa wa kombe hilo.

Collins Injera na William Ambaka, ambao walikuwa mashujaa katika ushindi wa 21-12 dhidi ya New Zealand kwenye nusu fainali, walilishwa kadi ya manjano.

Fiji ilitumia wingi wao uwanjani kufunga trai mbili kupitia kwa Eroni Sau na Amenoni na kuongezea kwa trai ya ufunguzi ya Josua Vakurunabili.

Fiji iliongoza 17-0 katika kipindi cha mapumziko katikafainali hiyo iliyokuwa marudio ya fainali ya Canada Sevens ambapo Fiji pia ilishinda 29-7.

Kenya ilijaribu kuwafuata Fiji kupitia mchezo wa kuridhisha uliomwezesha Billy Odhiambo kufunga, lakini trai ya Valemo Ravouvou ilipoteea Kenya imani.

Nahodha Oscar Ouma alijaribu kuonyesha uwezo wa Kenya kwa trai yake kupitia penalti, lakini maji yalikuwa yashamwagika kwa Shujaa.

You can share this post!

Dereva aliyemsaidia mama kujifungua atuzwa

Wakenya wengi wanapenda simu za Tecno – Utafiti

adminleo