• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 5:55 AM
Gharama hii ya harusi na mahari inaogofya vijana kuasi ukapera – Duale

Gharama hii ya harusi na mahari inaogofya vijana kuasi ukapera – Duale

Na GALGALO BOCHA

KIONGOZI wa wengi bungeni Aden Duale amelalamikia gharama kubwa ya harusi na mahari za jamii ya waislamu kuwa chanzo cha maelfu ya vijana kushindwa kuasi ukapera.

Akizungumza wakati wa sherehe ya kitamaduni ya jamii ya Wasomali eneo la Eastleigh, Bw Duale amesema vijana wengi waliofika umri wa kuoa, wanashindwa kuposa kwa hofu ya kutozwa mamilioni kama ada ya mahari.

Mbunge huyo wa Garissa Mjini alitoa mfano wa jamii yake ya Kisomali aliyosema imefika kiwango cha kuitisha dola 10,000 kama mahari kabla ya ndoa kufungwa.

“Gharama ya ndoa za kiislamu lazima ishukishwe. Kutaka vijana kulipa dola 10,000 ili kuoa ni kosa. Kama waislamu tumekosea na lazima kufanya ndoa kuwa nyepesi na isiyokuwa na gharama ili vijana waachane na mambo mengine ya kando kando,”

Alisema atakutakana na viongozi wa kidini haswa mashekhe wa msikiti wa Jamia, Nairobi, kuanzisha mchakato wa kupunguza mahari na gharama za harusi.

Alisema tatizo hilo limepelekea idadi kubwa ya vijana wa Kiislamu kukosa matumaini ya kuoa na badala yake kujihusisha na hulka ya mapenzi kinyume na mafunzo ya dini.

“Jambo la kuitisha mahari ya dola elfu kumi kabla ya kufungisha binti yako nikaa, kama kwamba unanunua gorofa au gari lazima ikomeshwe. Nitakwenda msikiti wa Jamia siku ya Ijumaa na kuzungumza na mashekhe tutafute suluhisho,” akaeleza Bw Duale katika sherehe hiyo iliyofanyika Shule ya Upili ya Eastleigh.

Alisema jamii ya waislamu imekiuka utaratibu wa dini kuhusu jambo la ndoa.

Kiongozi huyo ya walio wengi bungeni, alisema harusi nyingi zinatekelezwa kinyume na mafundisho ya Mtume Muhammad.

“Wakati wa Mtume, unaulizwa kama una jamvi na kibanda cha kuanzia maisha kama wana ndoa kabla ya harusi kufanyika. Siku hizi unaulizwa uko na dola ngapi,” akalalama.

Bw Duale alisema chanzo cha jamii yake ya Kisomali kufanya ndoa kuwa na ghama ilitokana na watu wanaoishi mataifa ya ughaibuni ambao hulipa mari kwa dola za kimarekani.

Vile vile, mkoani Pwani vijana wengi wamekuwa wakilalamikia kiwango kikubwa cha mahari inayoitishwa na familia za wasichana.

Vijana wanaofanya kazi njee ya nchi haswa maeneo ya Mashariki ya Kati ndio wanaolaumiwa kufanya gharama ya ndoa kuwa juu.

Vijana hao wanalipwa mahari ya juu kutokana na thamani ya sarafu za mataifa za kiarabu, Uingereza na Marekani miongoni mwa zingine.

Aidha mbunge huyo wa Garissa Mjini amewahimiza wanawake wa kiislamu kuzingatia kwa dhati vazi la hijab ambalo alisema ndilo pambo rasmi la waislamu kote duniani.

Aliwahimiza waume pia kuhakikisha wamewajibika katika ndoa na vile vile mke zaidi ya mmoja

 

You can share this post!

Hali si shwari: Waiguru ayumbishwa na kimbunga cha siasa

Mwanamke alilia haki kufuatia mateso Uarabuni

adminleo