• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 4:10 PM
Wataka bunge lipitishe sheria kulinda tiba za kiasili

Wataka bunge lipitishe sheria kulinda tiba za kiasili

Na TITUS OMINDE

MADAKTARI wa tiba za kiasili wanataka bunge kupitisha sheria kuhusu tiba hizo. 

Madaktari hao walisema kupitishwa kwa sheria hiyo kutakabiliana na matapeli katika sekta hiyo mbali nakutoa mazingira bora ya wahudumu wa tiba za kiasili.

Daktari Shadrack Moimet wa zahanati ya Koibatek mjini Eldoret alisema kukosekana kwa sheria na sera kuhusu tiba hizo kumechangia katika ongezekeo la matapeli katika tiba husika.

Dkt Moimet alisema iwapo wabunge watapitisha sheria hiyo Wakenya wataondoa dhana potovu kwamba tiba za kiasili ni uchawi.

“Ikiwa sheria hii itapitishwa matapeli ambao wamevamia sekta hii watadhibitiwa mbali na kuondoa dhana potovu kwamba tiba za kiasili ni ushirikina na uchawi.”

Anataka wahudumu katika tiba hizo kushirikiana ili kuona kwamba matakwa yao yanatekelezwa.

Mswada kuhusu tiba hizo umekuwa bungeni tangu bunge la tisa ambapo umekuwa ikihairishwa mara kwa mara.

Madaktari wa tiba za kiasli wanadai kuwa iwapo watapewa mazingira bora ya kuendelezea kazi zao watashirikiana na madaktari wa tiba za kisasa kukubiliana na changamoto ya maradhi tata.

“Dawa zetu zina uwezo wa kutibu ugonjwa kama vile saratani na maradhi mengine ambayo hayana tiba zakisasa, kile tunataka ni kutambuliwa na kushirikishwa vilivyo katika utafiti wa maradhi husika,” akasema.

Vile madaktari hao wanataka serikali kuwatengea fedha za kuendeleza utafiti kupitia tiba za kiasili kama ilivyo nchini Uchina.
 

You can share this post!

Vijana wapanga kuvumisha utamaduni

ODM yaionya Jubilee dhidi ya kuvuruga muafaka

adminleo