• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 11:55 AM
Mazungumzo baina ya Kanisa na vijana yachangia kuimarika kwa usalama

Mazungumzo baina ya Kanisa na vijana yachangia kuimarika kwa usalama

Na SAMMY KIMATU

KANISA linafurahia matunda ya mazungumzo na vijana yaliyochangia kuimarika kwa usalama wakati wa msimu wa sherehe.

Aidha, hakuna ripoti zilizotolewa kuhusiana na uhalifu Desemba 2019 katika maeneo ya Ngelani na Kisekini.

Akiongea mwishoni mwa wiki katika Kanisa la Africa Inland Ngelani katika Kaunti ya Machakos, Mchungaji Bonface Kyalo Nthenge alisema nidhamu ilisisitizwa kwa vijana kupitia mikutano na kambi.

“Kama kanisa, tunashirikisha vijana wetu katika kujikimu katika kambi za vijana na programu zingine za kanisa kupitia Idara ya Elimu ya Kikristo almaarufu CED,” Rev Nthenge aliambia Taifa Leo.

Alimshukuru mtoto wa kike kwa kuwapiku wavulana katika KCPE na KCPE na kuongeza kwamba wasichana walizoewa kwa kuonekana wadhaifu wakilinganishwa na wavulana.

“Siku za hapo nyuma, kasumba ilikuwa ni wavulana wanaongoza katika mitihani lakini wakati huu, mambo yamebadilika,” akasema.

You can share this post!

MATUKIO 2019: Watu mashuhuri walioacha pengo baada ya...

Korti yasitisha kuongezwa kwa ada ya kuegesha magari jijini...

adminleo