• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 5:15 PM
MAPISHI: Jinsi ya kuandaa viazi vya kuponda, kuku na sosi

MAPISHI: Jinsi ya kuandaa viazi vya kuponda, kuku na sosi

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa kupika: Dakika 20

Walaji: 3

Vinavyohitajika kwa viazi

  • kilo 1 ya viazi
  • lita 1 ya maji
  • maziwa ½ kikombe
  • vijiko 3 vya siagi
  • chumvi

Maelekezo

Menya, osha na kukatakata viazi vipande vikubwa vikubwa.

Weka viazi kwenye sufuria na ongeza maji ya kutosha.

Chemsha mpaka maji yachemke, kisha ongeza chumvi. Chemsha mpaka viazi viive vizuri.

Viazi vikishaiva vizuri, epua kisha chuja maji.

Anza kuponda viazi na uhakikishe hakuna mabonge mabonge.

Ongeza maziwa na siagi mpaka upate uzito na ladha utakayopenda.

Vinavyohitajika kwa kuku

  • kilo ½ minofu ya kuku
  • pilipili mboga 3 (nyekundu, kijani na njano)
  • kitunguu maji 1
  • mafuta ya kupikia
  • kijiko 1 cha chicken seasoning
  • kijiko 1 cha kitunguu saumu na tangawizi
  • chumvi na pilipili manga

Maelekezo

Andaa viungo kisha katakata kuku, kitunguu na pilipili mboga vipande virefu virefu.

Kwenye kikaangio katika moto wa wastani, chemsha mafuta, kisha ongeza nyama ya kuku, chicken seasoning, kitunguu saumu na tangawizi.

Kaanga mpaka nyama ikaribie kuiva, kisha ongeza kitunguu maji, pilipili hoho, chumvi na pilipili manga.

Endelea kukaanga kwa dakika chache, mpaka kuku iive vizuri.

Pakua na viazi vya kuponda,mboga na ufurahie.

You can share this post!

AC Milan pia yamezea mate Victor Wanyama

LISHE NA AFYA: Jinsi ya kuandaa smoothie ya stroberi na...

adminleo