• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 8:55 AM
MAPISHI: Jinsi ya kuandaa wali unaopendwa sana Afrika Magharibi

MAPISHI: Jinsi ya kuandaa wali unaopendwa sana Afrika Magharibi

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa kupika: Saa moja

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • kuku vipande 8
  • kitungu 1 kilichokatwakatwa
  • nyanya 3
  • kitungu saumu kilichomenywa
  • gramu 400 za ‘tomato paste’
  • gramu 400 za mchele wa Basmati uliopikwa kiasi kuwa wali
  • pilipili mboga 1 lakini nyekundu 1 iliyokatwa
  • curry powder kijiko nusu
  • chumvi kijiko
  • mafuta ya kupikia
  • maji vikombe 3

Maelekezo ya wali

Zimenye nyanya, pilipili mboga na kitunguu saumu.

Bandika sufuria mekoni,weka mafuta ya kupika. Acha yapate moto vizuri kisha weka vitunguu. Koroga hadi vianze kubadilika rangi. Ongeza tomato paste kisha kaanga kwa dakika tatu.

Ongeza nyanya zilizomenywa na ukaange kwa dakika 10. Hakikisha unakoroga kuepuka kuungua.

Baada ya dakika 10 punguza moto na uongeze chumvi, curry powder na viungo vingine upendavyo. yaache yachemke kwa dakika 10.

Ongeza wali uliokuwa umechemshwa kiasi na ukoroge pamoja na nyanya. Ongeza maji kiasi na ufunike baada ya kupunguza moto ili chakula kiive polepole kwa dakika 10 au hadi yaishe maji. Chakula kiko tayari.

Maelekezo ya nyama

Andaa nyama kwa kuiosha na uweke pembeni ichuje maji. Nyunyizia chumvi kiasi.

Bandika sufuria mekoni, weka nyama na ufunike ukishaipunguza moto ili yaive polepole bila maji kwa dakika 10.

Bandika sufuria nyngine na uweke mafuta ya kupika vikombe vitatu na uache yawe moto kabisa.

Vitumbukize vipande vya kuku kwenye mafuta na pinduapindua kwa dakika 15 hadi vibadilike rangi.

Sasa chakula chako kiko tayari.

You can share this post!

Muhiddin aelezea matumaini ya Bandari kung’aa KPL, FKF

Homa ya China yazua hofu

adminleo