Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 10
Muda wa kupika: Saa moja
Walaji: 4
Vinavyohitajika
Maelekezo ya wali
Zimenye nyanya, pilipili mboga na kitunguu saumu.
Bandika sufuria mekoni,weka mafuta ya kupika. Acha yapate moto vizuri kisha weka vitunguu. Koroga hadi vianze kubadilika rangi. Ongeza tomato paste kisha kaanga kwa dakika tatu.
Ongeza nyanya zilizomenywa na ukaange kwa dakika 10. Hakikisha unakoroga kuepuka kuungua.
Baada ya dakika 10 punguza moto na uongeze chumvi, curry powder na viungo vingine upendavyo. yaache yachemke kwa dakika 10.
Ongeza wali uliokuwa umechemshwa kiasi na ukoroge pamoja na nyanya. Ongeza maji kiasi na ufunike baada ya kupunguza moto ili chakula kiive polepole kwa dakika 10 au hadi yaishe maji. Chakula kiko tayari.
Maelekezo ya nyama
Andaa nyama kwa kuiosha na uweke pembeni ichuje maji. Nyunyizia chumvi kiasi.
Bandika sufuria mekoni, weka nyama na ufunike ukishaipunguza moto ili yaive polepole bila maji kwa dakika 10.
Bandika sufuria nyngine na uweke mafuta ya kupika vikombe vitatu na uache yawe moto kabisa.
Vitumbukize vipande vya kuku kwenye mafuta na pinduapindua kwa dakika 15 hadi vibadilike rangi.
Sasa chakula chako kiko tayari.