• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 6:50 AM
Njoki Ndung’u alivyojitetea katika kesi ya kuongoza mgomo

Njoki Ndung’u alivyojitetea katika kesi ya kuongoza mgomo

Na RICHARD MUNGUTI

JAJI wa Mahakama ya Juu Njoki Ndung’u  amejitetea katika kesi anayoshtakiwa Mahakama Kuu ya kuchochea mgomo kufuatia agizo la kustaafishwa kwa majaji wawili na Tume ya kuajiri watumishi wa idara ya Mahakama (JSC) baada ya kuhitimu miaka 70 miaka mitano iliyopita.

Kufuatia uhaba huo ilimlazimu aliyekuwa Jaji Mkuu Dkt Willy Mutunga afanye kikao cha dharura cha JSC kilichohudhuriwa na Jaji Ndung’u na Jaji Jackon Ojwang kueleza malalamishi yao na uhaba wa majaji wa kufanyakazi mahakama hii ya upeo.

Jaji huyo alisema utata ulikumba idara ya mahakama baada ya kufahamika Jaji Mutunga alikuwa anatazamia kustaafu na aitha naibu wake Jaji Kalpana Rawal ama Jaji Philip Tunoi walioteuliwa chini ya katiba ya zamani wastaafu wakiwa miaka 74 angelichukua wadhifa wa CJ.

Katika kizaazaa hicho Jaji Ndung’u alisitisha hatua ya kumstaafisha Jaji Rawal na JSC.

Wakati huo Jaji Mutunga alimruhusu Jaji Rawal kuongoza kamati ya majaji wa Mahakama ya Juu waliokuwa wamenusa hali ya hatari kwa vile majaji watatu walikuwa wastaafu. Majaji hao ni Jaji Mutunga, Rawal na Tunoi.

“ Mahakama ya Juu ilikuwa isalie majaji wanne tu na hakungekuwa na kazi yoyote ambayo ingelifanyika,” alisema Jaji Ndung’u.

Ni katika hali hiyo yeye na Jaji Ojwang waliandikia JSC barua wakiishutumu kwa kutaka kumstaafisha Jaji Rawal ilhali miaka yake ya kustaafu ilikuwa 74 na wala sio 70.

Barua ya kumstaafisha ilikuwa imetiwa sahini na msajili wa idara ya mahakama Annah Amadi…

Jaji Mutunga na Jaji Smokin Wanjala walikuwa wanachama wa kamati ya JSC na waliitisha kikao cha dharura cha tume hiyo kikutane na Majaji Ndung’u na Ojwang wakabiliane nalo kwa vile suala la kustaafishwa kwa Jaji Rawal na Tunoi lilikuwa la dharura na la manufaa makubwa kwa umma.

“ Hakukuwa na majaji wa kutosha wa kusikiza kesi katika mahakama ya juu,” Jaji Ndung’u alimweleza Jaji Weldon Korir anayesikiza ya kushtakiwa kwa jaji huyo mbele ya JSC na wakili Apollo Mboya.

Baada ya kikao cha pamoja JSC na Majaji Ndung’u na Ojwang anayestaafu mwezi huu (Februari 2020) walishtakiwa na aliyekuwa afisa mkuu wa chama cha mawakili nchini LSK Apollo Mboya akiomba Rais Uhuru Kenyatta ateue jopo la kuwachunguza majaji hao wawili kwa lengo la kuwatimua kazini.

Jaji Ndung’u alisema kulikuwa na uhaba wa majaji katika mahakama hii ya upeo “hata ikambidi asiende likizo ya kujifungua.”

Jaji huyo alisema hali ya suinto fahamu ilikuwa nyingi hata inadaiwa wawili hao walimshawishi jaji mwingine ajiunge nao kususia kazi.

Kesi yao ilisikizwa na JSC na wakakemewa wote wawili (Njoki na Ojwang).

Njoki anaomba uamuzi huo wa JSC wa kumshutumu ufutiliwe mbali.

Lakini wawili hao walidumisha msimamo wao wa kupinga kustaafishwa kwa wenzao kwa mujibu wa barua waliyoandika na kumshutumu Jaji Mutunga.

“Barua ya arifa ya kustaafishwa kwa aliyekuwa naibu wa Jaji Mkuu (DCJ) Kalpana Rawal na Jaji Philip Tunoi waliokuwa wamehitimu miaka 70 ilizuia hali ya suinto fahamu katika Mahakama ya Upeo,” alisema Jaji Ndung’u.

Jaji huyo aliyetoa ushahidi mbele ya Jaji Weldon Korir alisema kutokana na uhaba wa majaji katika mahakama hiyo ya upeo , ilimbidi aiandikie barabara JSC kuhoji suala hilo.

“Miktano baina ya Majaji wa Mahakama ya Juu (CJ) Dkt Mutunga, Jaji Rawal, Jaji Tunoi, Jaji Mohammed Ibrahim , Jaji Ojwang, Jaji Smokin Wanjala na Jaji Ndung’u ilifanywa mara kwa mara kujadilia uhaba wa majaji na utenda kazi katika mahakama hii ya upezo,” Jaji Korir alifafamishwa.

Wakati wa mikutano hiyo suala nyeti lililozuka na kustaafishwa kwa Majaji Rawal na Tunoi.

Wawili hawa walikuwa wamepinga kustaafishwa wakisema “ waliteuliwa kwa mujibu wa katiba ya zamani iliyokuwa inasema majaji watastaafu wakihitimu umri wa miaka 74.”

Majaji Ndung’u , Ojwang walilalamikia kuhusu utenda kazi ikitiliwa maanani ni majaji aidha watano ama sita wanaoweza kuendeleza kesi.

Wakati wa mikutano iliyofanywa , yeye (Njoki) alinunukuu masuala yaliyojadiliwa na mara kwa mara ubishi ulizuka kuhusu uhalali wa masuala yaliyojadiliwa.

“Licha Jaji Mutunga kumtea Jaji Rawal aongoze vikao na kumwarifu baada kilichoafikianwa,” alisema Jaji Ndung’u.

Jaji Ndung’u alikuwa akitoa ushahidi katika waliyoshtakiwa na aliyekuwa afisa mkuu katika chama cha wanasheria nchini Apollo Mboya aliyewashtaki kwa JSC na kuiomba impendekezee Rais Uhuru Kenyatta ateue jopo la kuwachunguza Majaji Ndung’u na Ojwang kuchochea mgomo baridi katika mahakama ya juu.

Hatimaye Majaji Rawal na Tunoi waling’atuliwa baada ya Mahakama ya Juu ikiongozwa na Jaji Mutunga kuamua umri wa kustaafu kwa majaji wa Mahakama ni miaka 70 kwa mujibu wa Katiba iliyopitishwa 2010.

Awali majaji hawa wawili waliwasilisha kesi mahakama kuu kuamua umri wa kustaafu.

Kesi hiyo ilisikizwa na mahakama kuu , mahakama ya rufaa na Mahakama ya Juu ambayo ilifikia uamuzi umri wa kustaafu ni miaka 70 na wala sio 74.

“Ijapokuwa kesi hii ilikuwa inaendelea mbele ya mahakama kuu na rufaa majaji wa mahakama ya juu walikutana kujadilia suala hilo la kustaafishwa kwa majaji wawili chini ya uenyekiti wa Jaji Mutunga na Jaji Rawal mtawalia,” alisema Jaji Ndung’u

Kabla ya mahakama ya juu kuamua Jaji Tunoi ang’atuke kulitokea mlalamishi aliyedai jaji huyo aliyekuwa na tajriba ya juu alikuwa ameumishwa mlungula wa Sh200milioni na Gavana Evans Kidero awashawishi majaji wengine wa mahakama ya juu kutupilia mbali kesi aliyokuwa ameshtakiwa na aliyekuwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu.

Mwaka wa 2013 Bw Waititu alikuwa amewania Ugavana Nairobi na kunyoroshwa na Dkt Kidero.

Waititu alihama Nairobi wakati huo na kuwania Ubunge wa Kabete baada ya kuuawa kwa aliyekuwa Mbunge George Muchai 2015.

Kashfa hiyo ya Jaji Tunoi ya ulaji rushwa ilimtoa pumzi hata akaamua kustaafu kabla ya Jaji Mutunga , Jaji Smokin Wanjala na Jaji Mohamed Ibrahim,

Majaji Ndung’u na Ojwang walitofautiana na uamuzi wa Majaji Mutunga, Wanjala na Ibrahim.

Ni kufuatia mtafaruku huu Bw Mboya aliomba JSC impendekezee Rais Uhuru Kenyatta ateue jopo la kuwatimua kazini majaji hao wawili Ndung’u na Ojwang kwa kuchochea mgomo wa mahakama ya juu.

Badala ya kupendekeza wachunguzwe JSC iliwashutumu na ni uamuzi huu Jaji Ndung’u anaomba upigwe kalamu na Jaji Korir.

Kesi inaendelea Jumanne.

You can share this post!

Gavana Nyoro huru kuteua naibu wake

Hatimaye serikali kumfidia Amrouche Sh108m

adminleo