• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 8:55 AM
FAO yaonya uvamizi wa nzige unahatarisha upatikanaji wa chakula

FAO yaonya uvamizi wa nzige unahatarisha upatikanaji wa chakula

Na MAGDALENE WANJA

SHIRIKA la Chakula na Kilimo (FAO) la Umoja wa Mataifa limetoa onyo likisema kwamba uvamizi wa nzige unaoshuhudiwa katika baadhi ya mataifa ya Afrika Mashariki ni tishio kubwa kwa upatikanaji wa chakula.

Kufikia sasa, mataifa yaliyoathirika zaidi ni pamoja na nchi za Ethiopia, Kenya, na Somalia na Uganda likiwa la hivi karibuni.

Katika taarifa iliyotolewa na shirika hilo, nzige wa jangwani ni tishio kubwa kwa upatikanaji wa chakula cha kutosha na kwa maisha ya watu katika eneo la Pembe ya Afrika.

“Mataifa ya Afrika Mashariki yamekekuwa yakikabiliana na nzige tangu mwaka wa 2020 kwa kile kinachotambuliwa kama uvamizi mbaya kuwahi kutokea katika eneo hilo,” ilisema taarifa hiyo.

Mtaalamu wa masuala ya mazingira na Afrika wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) Richard Munang aliyenukuliwa katika taarifa hiyo alisema kuwa mara nyingi, nzige wa jangwani huwa katika maeneo kame na jangwani.

Sehemu hizi ni pamoja na baadhi ya nchi barani Afrika, Maeneo ya Asia Mashariki na Kusini Mashariki mwa Asia.

“Haya ni maeneo ambayo hushuhudia kiwango cha mvua chini ya milimita 200 kila mwaka. Katika hali ya kawaida, idadi ya nzige hupungua kupitia kufa wenyewe au kwa kuhama,” alisema Bw Munang.

Kulingana na Bw Munang, hali ya hewa na tabianchi pia huvutia kuongezeka kwa nzige.

Kuongezeka kwa mvua kuliko kiwango cha kawaida kulishuhudiwa kwenye Pembe ya Afrika tangu Oktoba hadi Desemba mwaka wa 2019.

Alishauri kuwa wadudu hao wanaweza kudhibitiwa kwa kunyunyiziwa kemikali za oganofosfeti.

Nchini Kenya, zaidi ya kaunti 15 zimeathirika na nzige hao ambao wanazaana kwa kasi.

You can share this post!

SEKTA YA ELIMU: Serikali isifanye masihara na usalama wa...

NDIVYO SIVYO: ‘Mapua’ ni neno linalotumiwa...

adminleo