• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 6:50 PM
Hatimaye vibarua Pumwani kulipwa mshahara wa miezi 4

Hatimaye vibarua Pumwani kulipwa mshahara wa miezi 4

Na Collins Omullo

NI afueni kwa vibarua wanaohudumu katika hospitali ya kujifungulia kinamama ya Pumwani, baada ya Kaunti ya Nairobi kusema kuwa mishahara yao ya miezi minne italipwa kufikia Alhamisi, wiki hii.

Akizungumza na waandishi wa habari, Washington Makodingo, Afisa Mkuu katika idara ya mipango ya kiuchumi alisema kuwa mnamo Jumatatu, kaunti hiyo ilitenga Sh8 milioni kutoka kwa mkaguzi wa bajeti, ambayo itatumika kulipa mishahara ya vibarua hao ambayo haijalipwa kuanzia Novemba, mwaka jana.

“Tulipata ombi la mishahara iliyochelewa kulipwa siku ya Ijumaa, wiki jana. Hata hivyo, tumetuma ombi kwa mkaguzi wa bajeti atoe angalau Sh8 milioni. Ombi letu likikubaliwa, tutalipa vibarua hao,” akasema Bw Makodingo.

Mnamo Jumatatu, vibarua na wauguzi wote walioathiriwa walikuwa na mgomo baridi huku wakiagiza serikali iwalipe mishahara yao iliyochelewa tangu Novemba, mwaka jana.

Katika barua moja iliyoandikwa Januari 31, 2020, Afisa Mkuu idara ya afya katika Kaunti, Mohamed Sahal aliomba msimamizi wa hospitali ya Pumwani kurefusha mkataba wa wafanyikazi 285 hadi Februari 31, 2020.

 

You can share this post!

Sonko amkabidhi Uhuru usimamizi wa Nairobi

Coronavirus inavyohangaisha Wakenya

adminleo