• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
SENSA: Wakenya milioni 7 hawajasoma

SENSA: Wakenya milioni 7 hawajasoma

Na DIANA MUTHEU

WATU 7.1 milioni hawajawahi kuhudhuria shule hata siku moja, ripoti moja imeeleza.

Kulingana na matokeo ya Sensa ya mwaka wa 2019 yaliyotolewa Ijumaa iliyopita, kati ya watu 47.6 milioni humu nchini, asilimia 16.3 hawajawahi kuenda shuleni.

“Watu 7.1 milioni hawajawahi kuhudhuria shule,” ikasema ripoti hiyo ya Sensa iliyoandaliwa na Shirika la Takwimu Nchini (KNBS).

Katika ripoti hiyo watu wengi ambao hawajapata elimu, asilimia 19.6 walikuwa mashambani ambao ni 5.9 milioni huku na kwa jumla walikuwa 1.1 milioni.

Ripoti yenyewe ilieleza zaidi kuwa idadi ya wanawake ambao hawajawahi kuhudhuria shule ilikuwa juu zaidi kuliko ya wanaume na ile ya watu wenye jinsia mseto. Wanawake walikuwa asilimia 17.6 ilhali wanaume walikuwa asilimia 14.9.

“Idadi ya wanawake ambao hawana elimu ni 3.8 milioni na wanaume ni 3.2. Watu wenye jinsia mseto walichukua asilimia 20.7 kwa kuwa 207 miongoni mwao hawajawahi kuenda shuleni,” ikasema ripoti.

Vile vile, ripoti hii ilifafanua kwa undani zaidi kuwa watu wengi ambao hawana elimu wanatoka katika kaunti za Garissa, Wajir na Mandera. Kaunti hizi zinapatikana katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa nchi.

Kaunti ya Garissa inaongoza kwa idadi ya watu 5.8 milioni (asilimia 75.2) ambao hawana elimu, ikifuatiwa na Mandera ambao ni 5.5 milioni (asilimia 71.9) na kisha Wajir,5.4 milioni (75.2).

Kulingana na KNBS, katika kaunti za Garissa na Wajir, idadi ya wanaume ambao hawana elimu ni juu zaidi kuliko ya wanawake. Kaunti ya Garissa ni 311,556 (asilimia 73.2) na Wajir ni 285,684 (asilimia 75.3).

“Wanawake ambao hawajawahi kuhudhuria shule katika kaunti ya Garissa ni 273,149 (asilimia 77.5) ilhali katika kaunti ya Wajir ni 263,682 (79.4),” ikasema ripoti.

Katika kaunti ya Mandera, idadi ya wanawake ambao hawana elimu ni juu zaidi kuliko ya wanaume.

Wanawake ni 284,543 (asilimia 74.1) na wanaume ni 271,252 (asilimia 69.3).?Ripoti hii ilisema kuwa watu 18,750 nchini wanahudhuria elimu ya ngumbaru. Hata hivyo, wengi wao walikuwa wa mashinani.

“Watu walio katika miji na wanasoma ngumbaru ni 3,780 ilhali wale wa mashinani ni 14,970. Wanaume ni 9,561 na wanawake ni 9,187,” ikasema.

You can share this post!

SENSA: Simu nyingi nchini zinamilikiwa na wanawake

Sanamu za Sonko zaharibiwa jijini

adminleo