• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 1:15 PM
Papa Francis haugui virusi vya corona – Ripoti

Papa Francis haugui virusi vya corona – Ripoti

Na MARY WANGARI

BABA mtakatifu Francis, aliyefutilia mbali likizo ya Lenti kwa mara ya kwanza katika hatamu yake kama papa kwa sababu alikuwa anaugua, amepatikana bila virusi vya corona.

Hii ni kulingana na vyombo vya habari nchini humo vilivyoripoti mnamo Jumanne, Februari 3.

Msemaji wa Vatican Matteo Bruni alisema hakuwa na maoni wakati huo ripoti hiyo ilipotolewa,

Kiongozi huyo wa Kanisa la Katoliki la Roma mwenye umri wa miaka 83 aliyetolewa kijisehemu cha pafu lake moja kutokana maradhi miongo kadhaa iliyopita, pia alifutilia mbali sehemu kubwa ya mikutano wiki iliyopita.

Francis alitarajiwa kushiriki likizo hiyo ya wiki moja na maafisa wakuu wa Vatican iliyoanza Jumapili usiku katika kanisa moja kusini mwa Roma.

Lakini kupitia tangazo lililowapata wengi bila kutarajia saa chache baadaye, alisema atafuatilia shughuli hiyo kutoka chumba chsake cha wageni Vatican.

Ameripotiwa kuugua wakati ambapo taifa la Italia linakabiliana na mkurupuko unaozidi kusambaa wa virusi hatari vya corona.

Idadi ya vifo nchini Italia iliruka hadi 52 kutoka 34 siku iliyotangulia na jumla ya idadi iliyothibitishwa katika taifa lililoathiriwa zaidi barani Uropa ikipita kiwango cha 2,000.

You can share this post!

Corona sasa yasababisha uhaba wa shashi madukani

Waliotupwa jela kimakosa miaka 36 kufidiwa Sh297m kila mmoja

adminleo