• Nairobi
  • Last Updated March 18th, 2024 8:55 PM
Kero mitandaoni polisi kumuua Mwafrika kwa kumkanyaga shingoni kwa goti

Kero mitandaoni polisi kumuua Mwafrika kwa kumkanyaga shingoni kwa goti

NA MASHIRIKA

Minnesota, Amerika

Video ya Mwafrika aliyefariki baada ya polisi wa Minneapolis kumkanyaga kwa goti shingoni huku amemtia pingu kwa muda wa zaidi ya dakika tano imezua hamaki na kero mitandaoni, wengi wakitaja dhuluma za polisi wa rangi nyeupe kwa watu weusi kama kukithiri kwa ubaguzi wa rangi.

Meya wa Minneapolis Jacob Frey aliwapiga kalamu polisi wanne kufuatia kifo cha George Floyd, ambaye hakuwa amevalia shati katika barabara ya Minneapolis, huku afisa mmoja akimkatia hewa ya kupumua kwa kumkanyaga shingoni.

“Siwezi kupumua, siwezi kupumua…mama.mama,” Floyd alilia polisi huyo asimsikize kamwe na kuendelea kumdhulumu.

Waliokuwa wakitazama walirekodi video ya Flyod anayekisiwa kuwa na miaka 46 akizimia na kukosa pumzi na nguvu za kunena na kujipindua na mwishowe kukimywa huku maafisa hao wakimwamuru kusimama aingie kwenye gari .

Baadaye ambulansi ilifika mahali hapo na kumpeleka hospitalini ambapo alitangazwa kufariki.

“Nilichoona katika video hio kinachukiza sana. Kwa dakika tano tulimuona afisa Mzungu akifinyilia goti lake kwa shingo la mwanaume Mwafrika bila huruma,” Frey alisema.

“Kuwa Mwafrika haifai kuwa hukumu ya kifo.”

You can share this post!

Kuchezea Gor Mahia kuliniandaa kwa soka ya ushindani mkubwa...

COVID-19: Kenya yarekodi idadi ya juu zaidi ya visa vipya...

adminleo