• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:21 PM
Walimu wakuu wawapa wanafunzi barakoa

Walimu wakuu wawapa wanafunzi barakoa

NA WAWERU WAIRIMU

Walimu wakuu wa shule za upili katika Kaunti ya Isiolo wameanza kuwasambazia barakoa wanafunzi nyumbani kufuatia hatari inayowakodolea macho watoto hao ya kupatwa na ugonjwa wa corona kwa sababu wao hucheza kwa makundi nyumbani.

Walimu hao tayari wamewapa watoto zaidi ya 300 katika wadi ya Ngaremara barakoa na kuwaelimisha familia kuhusiana na jinsi ya kujikinga dhidi ya virusi vya corona.

Mwenyekiti wa Muungano wa Wakuu wa Shule za Upili tawi la Isiolo Abdi Diba alisema kwamba ni jambo la kusitikisha kuona watu wazima wakikijinga kutokana na corona huku wakiwaachilia watoto wao bila barakoa hali inayowaweka kwenye hatari ya kuambukizwa corona.

“Tunataka kuhakikisha kwamba wanafunzi wote walio nyumbani wamekingwa kutokana na virusi hivyo,” alisema Bw Diba. Walimu walilalamika kwamba familia nyingi hazina redio na hilo linalemaza masomo ya wanafunzi.

“Tuliwakuta wnafunzi 20 wakiwa wamekutana kwa familia moja kusikiliza redio, tunatafuta njia ya kuwasaidia wakati huu wako nyumbani,” alisema mkuu wa Shule ya Upili ya Wavulana ya Isiolo.

Bw Diba aliwaomba wazazi kuhakikisha wamewatunza watoto wao vizuri wakati huu wa corona na kuhakikisha hawataingizwa kwenye utumiaji wa dawa za kulevya.

You can share this post!

Aibu ya machifu kujinufaisha na chakula cha msaada

Madereva wamekuwa kisiki katika vita dhidi ya Covid-19...

adminleo