• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:58 PM
Mabaki ya kemikali ya usindikaji korosho yadhoofisha afya za wakazi wa Kiwapa

Mabaki ya kemikali ya usindikaji korosho yadhoofisha afya za wakazi wa Kiwapa

Na MISHI GONGO

WAKAZI zaidi ya 4,000 katika kijiji cha Kiwapa, Kaunti ya Kilifi wanaoishi karibu na eneo lililokuwa na kiwanda cha korosho cha Kenya Cashew Nuts Factory wanaendelea kuathiriwa na mabaki ya kemikali ya mafuta yaliyokuwa yakitumiwa katika usindikaji.

Wazazi wanaendelea kuishi kwa hofu ya watoto wao kuendelea kuchubuka ngozi hasa wanapoikanyaga ama kuigusa kemikali hiyo.

Tayari baadhi ya watoto wanauguza majeraha baada ya kuchubuliwa na kemikali hiyo.

“Watoto wetu wanauguza majeraha ya kuchubuka baada ya kukanyaga kemikali,” akasema Bi Kache Munga.

Aidha wakazi wana hofu kwamba huenda kukawa ya mkurupuko wa maradhi mbalimbali kufuatia ongezeko la mbu ambao wanaaminiwa kuletwa na kemikali hiyo.

Wameishinikiza Serikali kutafuta namna ya kulikabili suala hilo.

“Tunaomba serikali kutafuta njia ya kupunguza makali ya kemikali katika eneo hili. Tunahofia kuzuka kwa maradhi ya kukohoa na ngozi,” akasema Bw Ali Mzuri ambaye ni mkazi katika eneo hilo.

Kiwanda hicho kilisitisha shughuli mwaka wa 1995 baada ya kuhudumu kwa miaka ishirini.

Hata hivyo, wanasema kufikia leo hii athari za kemikali bado ziko katika mazingira; hewani na ardhini.

You can share this post!

Bayern Munich waingia fainali ya German Cup

Visiwa vya Mombasa na Manda huenda vikazama –...

adminleo