• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Watu 6 wajeruhiwa katika ajali ya ndege Meru

Watu 6 wajeruhiwa katika ajali ya ndege Meru

NA JACOB WALTER

Watu sita walipata majeraha baada ya ndege ya polisi iliyokuwa imebeba maafisa wa usalama kuanguka eneo la Kaithe, Kaunti ya Meru Jumamosi asubuhi.

Kamanda wa polisi eneo la Meru Patrick Lumumba alisema kwamba maafisa hao walikuwa wanaelekea katika mkutano wa usalama Marsabit.

Ndege hiyo ilitua kwenye shamba la ndizi. Wakazi walisaidia kutoa abiria kwenye ndege hiyo. Walioumia walikimbizwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Meru.

Maafisa wa usalama wa eneo hilo wamekuwa wakijaribu kudumisha usalama eneo la Badan Arero baada ya kikundi cha watu kutoka Marsabit kuvuka mpaka na kuingia Wajir na kuiba mifugo zaidi ya 70, na hali hiyo ikachochea vita kati ya jamii hizo mbili.

Watu wanne waliuawa katika vita hivyo Jumatatu.

Maafisa walikuwa wamepanga mkutano Jumamosi wa kurudisha usalama kati ya jamii hizo mbili. Mifugo waliokuwa wamebwa waliikuwa warudishwe kwa wenyewe mbele ya maafisa wa usalama wa eneo hilo, viongozi wa eneo hilo na wazee wa jamii hiyo.

Ajali hiyo ya ndege ilileta kumbukumbu za ndege iliyopata ajali Aprili 10, 2006 eneo la Marsabit ambapo watu kumi na moja wakiwemo wabunge sita walifariki.

You can share this post!

Mercy Cherono afanyiwa upasuaji wa mguu

Ng’ombe 24 wa mbunge wafa baada ya kula chakula hatari

adminleo