• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
Msanii Omondi Long Lilo kuzikwa leo

Msanii Omondi Long Lilo kuzikwa leo

NA DICKENS WESONGA

Mwanamziki maarufu wa Benga Erick Omondi Odit anayejulikana kwa jina la kisanii Omondi Long Lilo atazikwa Ijumaa nyumbani kwao Bondo baada ya serikali ya kaunti kupinga ombi la familia la kumzika Jumatano wiki ijayo.

Uamuzi huo ulifikiwa baada ya mkutano wa saa mbili uliofanyika kati ya familia ya mwanamziki na serikali ya kaunti katika makao makuu ya kaunti hio Jumatano.

Serikali ya kaunti ilisisitiza kwamba Long Lilo lazima azikwe Ijumaa huku wakilipa gharama ya chumba cha kuhifadhi maiti, na gavana Cornnell Rasanga akiwapa Sh30,000 za kununua jeneza.

Msemaji wa serikali ya kaunti Olima Gondi alisema kwamba watafuata maagizo ya serikali kwa sababu hawataki mazishi ya utata.

Alisema kwamba serikali inaendelea kulipa Sh160,000 wanazodaiwa baada ya marehemu kulazwa hospitalini kwa miezi miwili katika Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Bondo.

Kifo cha mwanamziki huyo wa miaka 37 kiliwacha ulingo wa usanii na kijiji kizima cha Gombe kwenye majonzi mapema wiki hii.

Msanii huyo alitajwa kuwa mpole, mchapakazi na aliyependa marafiki.

Kifo cha mwanamziki huyo kinajiri siku chache baada ya kifo cha mwanamziki Benard Onyago aliyejulikana kama Abenny Jachiga aliyezikwa usiku wa manane kufuatia mzozo wa mzishi yake kati ya polisi na wafuasi wake.

You can share this post!

Hofu ya ‘Jicho Pevu’ akitaka kung’oa...

Uhuru apigwa breki na mahakama

adminleo