• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Kutazama Elijah Manangoi na nduguye wakimenyana? Utasubiri zaidi

Kutazama Elijah Manangoi na nduguye wakimenyana? Utasubiri zaidi

Na GEOFFREY ANENE

WAPENZI wa riadha watalazimika kusubiri zaidi kuona ndugu na mabingwa wa duani Elijah Manangoi na George Manangoi wakitoana jasho katika mbio moja.

Hii ni baada ya Wakenya hawa wa dunia kuingia vitengo tofauti vya mbio katika duru ya kwanza ya Riadha za Diamond League itakayoandaliwa jijini Doha nchini Qatar mnamo Mei 4, 2018.

George atawania taji la mbio za mita 1500 naye Elijah ameamua kutimka katika mbio za mita 800.

George, ambaye ni bingwa wa dunia kwa wakimbiaji wasiozidi umri wa miaka 18, atakabiliana na Wakenya wenzake Bethwell Birgen, Collins Cheboi, Vincent Kibet, Jackson Kivuva, Andrew Rotich, Charles Simotwo na Justus Soget pamoja wakiambiaji kutoka Morocco, Canada, Australia, Qatar na Ethiopia.

Bingwa wa Riadha za Dunia za Watu wazima na Jumuiya ya Madola wa mbio za mita 1500 Elijah Manangoi, atashindania taji la mbio za mita 800 dhidi ya Wakenya wenzake Ferguson Rotich, Emmanuel Korir na bingwa wa dunia kwa wakiambiaji wasiozidi umri wa miaka 20 Kipyegon Bett na raia wa Burundi, Antoine Gakeme, ambaye ni mshindi wa medali ya fedha ya mbio hizi za mizunguko miwili katika Riadha za Ukumbini.

Wakali Bram Som (Uholanzi) na Adam Kszczot (Poland) wako katika orodha ya wakimbiaji 11 watakaowania ubingwa wa kitengo hiki.

You can share this post!

‘YouTube Man’ alenga kufufua makali yake...

Kibarua kwa Obiri mita 3,000 Diamond League

adminleo