• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
LISHE: Supu ya nyanya

LISHE: Supu ya nyanya

Na MARGARET MAINA

[email protected]

KATIKA kipindi hiki cha baridi kali, supu ya aina tofauti ni muhimu hasa unapotaka kinywaji kitakachokushibisha na kukupa joto linalohitajika.

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Muda wa kupika: Dakika 15

Wanywaji: 5

Nyanya zilizoiva. Picha/ Margaret Maina

Vinavyohitajika

  • nyanya 10 au zaidi zilizoiva vizuri
  • mafuta ya mzeituni vijiko 2
  • vitunguu saumu vipande 5
  • kitunguu maji 1
  • pilipili mboga 3 za rangi nyekundu
  • karoti 2
  • chumvi
  • curry powder
  • vegetable broth vikombe 4
  • juisi ya limau kijiko 1
  • asali kiasi
Nyanya zilizoiva zikiwa zimekatwakatwa. Picha/ Margaret Maina

Maelekezo

Osha nyanya na chemsha kwa muda wa dakika tano hadi uone ngozi ya juu inajikunja kasha toa katika maji na weka pembeni zipoe.

Baada ya kupoa toa maganda na katakata utie pembeni.

Chukua kikaangio kikubwa tia mafuta halafu yakichemka, tia kitunguu saumu na kitunguu maji na kanga kwa muda wa dakika mbili.

Weka pilipili mboga na karoti kisha kanga kwa dakika tano au hadi ziwe laini na kuiva. Nyunyuzia chumvi na uongeze nyanya ulizokatakata.

Weka broth,curry powder, asali na limau kasha chemsha kwa dakika 15 halafu toa na saga katika blenda. Baada ya hapo, supu yako itakuwa tayari.

Pakua na ufurahie.

Supu ya nyanya. Picha/ Margaret Maina

Waweza kunywa wakati wowote na mkate, na tena waweza kunywa ama ikiwa baridi au ikiwa ya moto.

Ikiwa wewe ni mpenzi wa nyama, waweza tumia nyama ya kusaga; tengeneza viduara vidogo na utatia katika hatua ya mwisho baada ya kuchanganya viungo vingine vyote.

You can share this post!

UOKAJI: Biskuti zenye ladha ya machungwa

NUSU-FAINALI FA: Manchester United kuvaana na Chelsea huku...

adminleo