• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 12:15 PM
Gor itapigana kufa kupona dhidi ya USM Alger – Shakava

Gor itapigana kufa kupona dhidi ya USM Alger – Shakava

Na JOHN ASHIHUNDU

Nahodha wa Gor Mahia, Harun Shakava amesema kuwa anatarajia mechi ngumu dhidi ya USM Alger, Jumatano.

Gor watakabiliana na klabu hiyo ya Algeria ugani Kasarani katika pambano la marudiano la CAF Confederations Cup katika Kundi D.

Kulingana na nyota huyo wa zamani wa klabu ya Kakamega Homeboyz alisema wenyeji wako katika hali nzuri baada ya kucheza mechi kadhaa mfululizo.

“Tumecheza mechi kadhaa ambazo zimetupa ujuzi wa kutosha kukabiliana na upinzani wowote ule…tutakuwa nyumbani mbele ya mashabiki wetu, na tutapigania ushindi kwa vyovyote vile,” Shakava aliongeza.

Mabingwa hao wa ligi kuu nchini walionyesha kiwango cha juu katika mechi ya kupimana nguvu dhidi ya Hull City, Jumapili kabla ya kushindwa 4-3 kupitia kwa mikwaju ya penalti, zilizoagana 0-0.

You can share this post!

Migne aita wengine wanne kuimarisha kikosi cha Stars

Sikuiba moyo wa mfu, mpasuaji ajitetea

adminleo