• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 3:34 PM
Sonko apinga kesi ya Sh1.7 bilioni

Sonko apinga kesi ya Sh1.7 bilioni

Na RICHARD MUNGUTI

GAVANA  Mike Mbuvi Sonko Jumatano aliomba mahakama kuu itupilie mbali kesi aliyoshtakiwa  na mwakilishi wa wadi ya Makongeni (MCA) Bw Peter Imwatok anayepinga bima ya afya ya Sh1.7 bilioni.

Wakili Harrison Kinyanjui alimweleza Jaji Hedwiq Ong’udi kuwa kesi aliyoshtaki  Bw Imwatok ilifaa isikizwe na kuamuliwa na  kamati ya kusimamia zabuni.

Bw Kinyanjui aliomba mahakama itupe kesi hiyo iliyoshtakiwa na Bw Imwatok akisema “ hajawasilisha ushahidi wowote kuthibitisha utoaji zabuni  ya huduma za afya kwa wafanyakazi wa kaunti ya Nairobi ulifanywa kwa njia isiyofaa.”

Pia Bw Kinyanjui alieleza Jaji Ong’undi kwamba MCA huyo wa wadi ya Makongeni alistahili kuwasilisha malalamishi yake kwa kamati inayohusika na masuala ya utoaji zabuni kwa kaunti.

MCA huyo analaumu  usimamizi wa Bw Sonko kwa kutumia vibaya pesa za umma ikiwa atalipa ada ya Sh1.7 bilioni.

Kesi hiyo itasikizwa mnamo Juni 7, 2018.

You can share this post!

Kesi ya jaji aliyetupa kesi iliyomkabili Pattni kusikizwa...

Huenda City Hall ikaadhibiwa vikali na Kenya Power

adminleo