• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
UTALII: Mkiendelea kuiga wenzenu mtatimua watalii

UTALII: Mkiendelea kuiga wenzenu mtatimua watalii

Na BERNARDINE MUTANU

Kampuni na mashirika ya kitalii yametakiwa kufanya mambo kwa njia tofauti kwa lengo la kuvutia watalii zaidi.

Wataalamu wamesema kuwa baadhi ya changamoto zinazoshuhudiwa na mashirika hayo yanatokana na kuiga yanachofanya mashirika mengine.

Kulingana na Tume ya Kitalii Ulimwenguni, mwaka 2017 idadi ya watalii ulimwenguni ilikuwa ni 1.2 bilioni ambapo 62 milioni walizuru Afrika.

Kulingana na takwimu kutoka shirika hilo, nafasi 8.3 milioni za kazi ziliundwa wakati wa kipindi hicho katika sekta ya utalii barani Afrika.

Katika mkutano uliofanywa Afrika Kusini, Durban, wataalamu wakiongozwa na Waziri wa Utalii Afrika Kusini Derek Hanekom waliwataka washikadau kutafuta njia za kukabiliana na changamoto na kuunda mazingira shwari ya kitalii.

You can share this post!

Airtel yalemewa na biashara Afrika, yapanga kung’atuka

Wakenya sasa wachangamkia mashangingi

adminleo