• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 9:55 AM
KEBS kuharibu bidhaa za thamani ya Sh250 milioni kwa kukosa ubora

KEBS kuharibu bidhaa za thamani ya Sh250 milioni kwa kukosa ubora

Na BERNARDINE MUTANU

BIDHAA za thamani ya Sh250 milioni humu nchini zitaharibiwa baada ya kukataa kufikisha upeo wa ubora.

Bidhaa hizo zilizo katika kontena 163 zilikuwa ni pamoja na tairi, spaghetti, mchele. Zilitengwa baada ya Shirika la kutathmini ubora wa bidhaa (KEBS) kusema hazikufikia ubora unaohitajika.

Kulingana na shirika hilo, mchele ulikuwa umeharibika baada ya kufikisha siku ya mwisho ya uuzaji. Spaghetti kwa upande wake hazikuwa zimefikia ubora unaohitajika na KEBS, baada ya uchunguzi wa mahabara.

Tairi zilizuiliwa kwa sababu Kenya huwa haikubali tairi kukuu hazikubaliwi nchini,” alisema meneja Mkurugenzi wa KEBS Charles Ongwae.

Wafanyibiashara wamekuwa na wakati mgumu forodhani kuirai KEBS kukubalia bidhaa zao humu ikiwa hawajapitia utaratibu uliowekwa na shirika hilo.

Bidhaa zote zinazoingia humu nchini zinakaguliwa eneo zinakotoka kwanza na kuwekewa kiwango cha ushuru na shirika hilo.

Hatua hiyo ni kwa lengo la kuzuia ukwepaji wa ushuru.

You can share this post!

Kiwanda kipya cha Coca-cola kupunguza ukosefu wa ajira

Je, maji haya yatapunguza gharama ya umeme?

adminleo