• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 8:50 AM
LISHE: Jinsi ya kuandaa ‘chickpea curry’

LISHE: Jinsi ya kuandaa ‘chickpea curry’

Na DIANA MUTHEU

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Vinavyohitajika

  • kitunguu 1
  • kitunguu saumu kipande 1 kubwa
  • tangawizi 1 iliyosagwa
  • mafuta ya kupikia vijiko 2
  • dania
  • pilipili mboga kipande ½
  • kijiko 1 cha Curry powder
  • chumvi
  • kikombe 1 cha chickpeas (zilizochemshwa)
  • tui (maziwa ya nazi) kikombe ½
  • sufuria
Vinavyohitajika kuandaa ‘chickpeas curry’. Picha/ Diana Mutheu

Jinsi ya kuandaa

Kata kitunguu chako, saga kitunguu saumu na tangawizi.

Katika sufuria, pasha mafuta yako moto kisha uongeze kitunguu na ukipike kwa moto wa wastani hadi kigeuge rangi. Ongeza kitunguu saumu, tangawizi, nyanya na pilipili mboga; koroga hadi viive vizuri.

Ongeza curry powder yako, dania na chickpeas. Funika sufuria na uwache mchanganyo huo uive kwa muda wa dakika tano.

Mimina maziwa ya nazi, koroga hadi ishikamane vizuri. Epua.

Waeza kuandaa kwa wali au chapati. Jiburudishe.

 

You can share this post!

Viongozi washauriwa kuwajali wananchi kwanza

Alvaro Morata arudi Juventus kwa mkopo kutoka Atletico...