• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Misikiti yaagizwa ipeperushe bendera, ifunze waumini kuhusu chama tawala

Misikiti yaagizwa ipeperushe bendera, ifunze waumini kuhusu chama tawala

Na AFP na VALENTINE OBARA

BEIJING, UCHINA

MISIKITI yote imeagizwa kupeperusha bendera za kitaifa ili “kuonyesha moyo wa uzalendo” miongoni mwa Waislamu.

Kulingana na Chama cha Uislamu Uchina ambayo ni idara ya kiserikali, bendera hizo zinafaa kupeperushwa mahali ambapo zinaonekana vyema msikitini.

Hatua hii “itaimarisha zaidi uwezo wa kuelewa maadili ya kitaifa na ya umma, na kueneza moyo wa uzalendo miongoni mwa Waislamu wa makabila yote,” kwa mujibu wa taarifa ya chama hicho.

Misikiti pia inahitajika kubandika wazi maelezo kuhusu misimamo ya chama tawala cha Communist, na kueleza waumini wao jinsi misimamo hiyo inavyowiana na maandiko ya dini ya Kiislamu ili ikite mizizi moyoni mwa waumini.

Chama cha Uislamu Uchina ni shirika la kiserikali lililo na mamlaka ya kuidhinisha Maimamu.

Barua hiyo ilizidi kusema kuwa wafanyakazi misikitini wanafaa kuandaa kuwe na mafunzo kuhusu katiba ya Uchina na sheria nyingine muhimu, hasa sheria mpya ya dini iliyofanyiwa mabadiliko hivi majuzi.

Chama hicho kilidai kuwa lengo kuu ni kufanya misikiti iwe maeneo ya elimu kuhusu chama tawala na sheria za nchi mbali na kuwa maeneo ya ibada na hivyo basi kuwezesha Waislamu wawe wazalendo.

Kuna Waislamu karibu milioni 23 nchini Uchina na dini hiyo ni miongoni mwa tano zinazotambuliwa rasmi na Chama cha Communist ambacho inahusishwa na wasioamini Mungu.

You can share this post!

Mvutano baina ya Ingwe na FKF kuhusu debi ya Mashemeji

Ndani miaka 30 kwa kumuua mfugaji

adminleo