• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Wazee wakemea matamshi ya chuki

Wazee wakemea matamshi ya chuki

Na Oscar Kakai

BARAZA la wazee wa jamii ya Kalenjin (Myoot) limetadharisha wanasiasa wa mirengo ya Kieleweke na Tangatanga dhidi ya kutoa matamshi ya chuki yanayoweza kutumbukiza nchi katika ghasia.

Wazee hao wametaka malumbano ya siasa za urithi wa urais mwaka 2022 yakome.

Mwenyekiti Bw James Lukwo alisema wanahofia kuhusu viongozi ambao wanatoa semi za chuki kiholela na kuendeleza ukabila ambao huenda ukaligawanya taifa.

Akiongea na wanahabari mjini Kapenguria, Bw Lukwo alisema wameshuhudia mambo yanayoweza kuibua uhasama kati ya jamii wakati wa uchaguzi.

“Tumekuwa tukifuatilia kwa makini matamshi ya wanasiasa. Tunataka yafike kikomo baada ya Rais kukutana na naibu wake wiki jana,” akasema, akigusia maombi ya kitaifa yaliyofanyika Ikulu ya Nairobi juzi.

 

You can share this post!

Wafuasi wa Ruto wasema hawatatishika

Shule zafunguliwa kwa tahadhari