• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 5:41 PM
LISHE: Keki ya vanilla isiyo na mayai

LISHE: Keki ya vanilla isiyo na mayai

NA WANGU KANURI

Jinsi ya kuandaa keki

Muda wa kuandaa: dakika kumi

Muda wa kuoka: dakika thelathini

Viungo

  • Vikombe vitatu vya unga wa ngano
  • Kikombe kimoja cha sukari
  • Kijiko nusu cha chai cha chumvi
  • Kikombe kimoja cha mafuta ya kupika
  • Viikombe viwili vya maziwa iliyoganda ama maziwa kawaida
  • Vijiko viwili vya kulia vya unga wa kuoka
  • Vijiko vinne vya chai vya vanilla
  • Kikombe kimoja cha sukari laini (icing sugar)
  • Kijiko kimoja cha chai cha maziwa
  • Chakuleti iliyoyeyuka

Maelekezo

  • Pasha tanuri yako kwa moto wa nyuzi 170.
  • Changanya unga, sukari, na chumvi pamoja. Hakikisha umechanganya vizuri.
  • Ongeza viowevu kwenye mchanganyiko wako. Viowevu hivyo ni mafuta ya kupika, maziwa
  • yaliyoganda na vanilla. Hakikisha umechanganya vizuri lakini sio sana. Mtiririko usiwe laini
  • sana.
  • Paka majarini kwenye bakuli ya kuokea kisha umimine mchanganyiko huo kwenye bakuli hiyo.
  • Oka kwa muda wa dakika thelathini.
  • Baada ya keki kupoa, changanya kikombe kimoja cha sukari laini na kijiko kimoja cha maziwa
  • kisha mwaga kwenye keki.
  • Unaweza kuongeza chakuleti iliyoyeuka kwenye keki yako.

You can share this post!

Hofu nyumba kumi zikibomolewa Isiolo

Fistula inavyowahangaisha wanawake