• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 6:50 AM
Wasagaji unga walia wanunuzi kupungua

Wasagaji unga walia wanunuzi kupungua

Na BARBANAS BII

KAMPUNI kadhaa za kusaga unga Magharibi mwa Kenya, zinakabiliwa na hatari ya kufunga biashara zao baada ya wanunuzi wengi wa unga kuacha kununua bidhaa hiyo na kuamua kutumia unga unaosagwa katika vinu vya kawaida, wanaoamini kuwa salama.

Watu wengi wanahofia unga unaosagwa viwandani una sumu ya aflatoxin kutokana na kiwango ambacho serikali ya Kenya imetoa kizingatiwe.

Hii ina maana kuwa baadhi ya wafanyakazi katika kampuni hizi watapoteza ajira.

Kampuni 10 ndogo ndogo za usagaji tayari zimewatuma baadhi ya wafanyakazi wao katika likizo ya lazima kutokana na ukosefu wa soko kwa bidhaa zao.

“Kwa kipindi cha majuma mawili yaliyopita hatujafanya kazi kikamilifu kwa sababu wanunuzi wanakataa unga gredi 1. Hali hii imetulazimisha kusitisha baadhi ya kanuni za serikali kuhusu kiwango cha aflatoxin kinachohitajika mahindi kuwa salama.

Wanasema mahindi mengi yanayozalishwa nchini yana kiwango cha aflatoxin kinachopelekea mazao hayo kutochukuliwa kuwa salama kwa matumizi ya binadamu.

Kulingana na wakurugenzi wa kampuni hizo, mahindi yanayozalishwa katika sehemu nyingi nchini yana kiwango cha aflatoxin ya punje 12 kwa kila punje bilioni ya mahindi. Wanataka viwango salama vya inflatoxin vilegezwe kwenda sambamba na viwango vinavyokubalika kimataifa.

Kupitia Muungano wa Wasagaji Nafaka (GBMA), kampuni hizo pia zimelalamikia uhaba wa mahindi kutokana na kupungua kwa uzalishaji msimu uliopita-kutoka magunia milioni 444 hadi magunia milioni 33. Aidha, wanataja kero la sumu ya aflatoxin kuwa changamoto kuu kwa shughuli zao.

“Wakati huu tumepunguza kiwango cha uzalishaji hadi asilimia 30 kutokana na uhaba wa mahindi, hali iliyosababishwa na changamoto ya uwepo wa kiwango cha juu cha aflatoxin,” akasema mwenyekiti wa GBMA Kipngetich Mutai.

Muungano huo ambao unaleta pamoja zaidi ya kampuni 35 za wasagaji wadogo, umeitaka serikali kulegeza kanuni kuhusu kiwango cha aflatoxin kinachochukuliwa kuwa salama kutoka 10 hadi 20 kwa bilioni moja ya punje za mahindi.

“Mexico ina viwango vya 20, China (40), Misri (30) na Korea Kusini (20). Viwango vyetu vikipunguzwa hadi 20, tutaweza kushindana vizuri katika soko huru,” akaongeza Bw Kipngetich.

You can share this post!

Wazee wa Kaya kujenga kituo kuenzi Mekatilili

MWALIMU KIELELEZO: Elizabeth Kadzo Ziro wa Shule ya Utange,...