• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 2:10 PM
Biden kutaja baraza lake la mawaziri Jumanne

Biden kutaja baraza lake la mawaziri Jumanne

Na AFP

WASHINGTON D.C., Amerika

RAIS mteule wa Amerika Joe Biden Jumanne, Novemba 24, 2020, atataja majina ya wale watakaohudumu katika baraza lake la mawaziri, msimamizi mkuu wa afisi yake ametangaza.

Hii ni licha ya kwamba Rais Donald Trump angali anakataa kutambua ushinda wa Biden licha ya kwamba baadhi ya wandani wake wameanza kuutambua ushindi wa mgombeaji huyo wa chama cha Democrat.

Rais huyu mteule ameendelea na matayarisho ya kuapishwa kwake mnamo Januari 20, hata baada ya Trump kuonyesha dalili za kukataa kuidhinisha matumizi ya fedha za umma kufadhili shughuli hiyo.

“Mtawajua wale ambao watateuliwa na Biden katika baraza lake la mawaziri kuanzia Jumanne,” afisa huyo kwa jina, Ron Klain, aliambia makala ya “This Week” (Wiki Hii) yaliyopeperushwa na shirika la habari la ABC Jumapili.

Mashirika kadha ya habari nchini Amerika, yakiwemo Bloomberg na gazeti la The New York Times, yaliripoti kwamba Biden atamteua mwanadiplomasia na mshirika wake wa miaka mingi, Antony Blinken, kuwa Waziri wa Masuala ya Kigeni.

Rais huyo mteule pia alisema wiki jana kwamba amefikia uamuzi kuhusu ni nani atamteua kuwa Waziri wa Fedha.

Vyombo vya habari nchini humo pia vilibashiri kuwa Biden atamteua Linda Thomas-Greenfield, ambaye alihudumu kama Naibu Waziri anayesimamia masuala ya Afrika katika utawala wa Rais wa zamani Barack Obama, kuwa Balozi wake katika Umoja wa Mataifa (UN).

Idadi kubwa wa viongozi wa Republican wametambua ushindi wa Biden au wametoa wito kwa idara ya General Servive Administration (GSA), itoa fedha za kufadhili hafla ya kumpokeza Bidens mamlaka.

Kwa kuwa Trump amedinda kutambua ushindi wa Biden, Rais huyo mteule amezuiwa kupata habari muhimu kuhusu sera za nyumbani na kigeni, haswa kuhusu janga la corona ambalo limeathiri pakubwa taifa hilo.

You can share this post!

ODONGO: Ubinafsi wa ODM kubana hela za vyama vya kisiasa

Ruto arejea nchini baada ya ziara ya Dubai