• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:55 AM
Pendekezo wafisadi wote wasukumwe jela maisha

Pendekezo wafisadi wote wasukumwe jela maisha

Na HAMISI NGOWA

MBUNGE wa Likoni, Bi Mishi Mboko amependekeza watu wanaopataikana na hatia ya ufisadi wafungwe gerezani maisha na kisha mali zao kutwaliwa na serikali.

Anasema ni kupitia kwa adhabu kali kama hiyo ambapo taifa hili litaweza kufaulu kwenye vita vyake dhidi ya ufisadi.

“Wakati umefika kwa taasisi za kisheria ikiwemo Idara ya Mahakama kuhakikisha zinawapa adhabu kali wanaopatikana na hatia ya ufisadi ili kuwa mfano kwa wenye hulka hiyo,” alisema.

Akizungumza mwishoni mwa wiki akiwa Likoni, mbunge huyo wa chama cha ODM alikemea vikali sakata ya mpya ya ufisadi iliyofichuliwa hivi majuzi katika Shirika la Vijana wa Huduma kwa Taifa (NYS) pamoja na ile ya mahindi akisema zinalemaza ajenda nne kuu za serikali.

Alisema inasikitisha kuona idara hiyo muhimu inayotegemewa kumaliza matatizo ya vijana ikihusishwa tena na sakata kubwa ya wizi wa mabilioni ya pesa.

“Ninaona wakati umefika kwa sheria kali kuchukuliwa dhidi ya watu wanaopatikana na hatia ya uporaji  mali ya umma. Wanafaa wafungwe gerezani maisha na mali yao kutaifishwa na serikali,” akasema.

 

You can share this post!

Maafisa 117 watumwa kwa ofisi za ubalozi ugenini

Jamii yahimizwa kukoma kuficha watu walemavu

adminleo