• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Waziri na wabunge 13 watoa Sh1,216 pekee kwa mchango

Waziri na wabunge 13 watoa Sh1,216 pekee kwa mchango

KIBOGA, UGANDA

Na JOSEPH KATO

WAKAZI wa kijiji cha Kibiga, Wilaya ya Kiboga, walipigwa na butwaa Jumanne wakati Waziri wa Jinsia, Peace Mutuuzo, akiandamana na wabunge 13 na maafisa wa utawala wa Kiboga walipotoa mchango wa Sh1,216 pekee (Sh45,000 za Uganda) kwa mwanamke mkongwe anayelea wajukuu zaidi ya 10 mayatima.

Pesa hizo zillikabidhiwa kwa nyanya huyo mwenye umri wa miaka 80, Teresa Namuli, na waziri pamoja na kilo mbili za sukari na mikate.

“Mimi si waziri lakini nikiwa na pesa, kile kiwango kidogo zaidi ninachoweza kutoa ni Sh270 (Sh10,000 za Uganda) au ninunue bidhaa mbalimbali niwape watu. Sielewi jinzi wabunge na mawaziri wanaweza kutoa pesa kidogo hivyo kwa familia yenye mahitaji mengi,” akasema mkazi, Robert Katumwa.

Bi Namuli anaishi kwenye nyumba ya matope iliyozeeka na baadhi ya wajukuu wake wamecha kwenda shuleni kwa sababu hawana uwezo wa kugharamia masomo.

Imekusanywa na Valentine Obara

You can share this post!

Mbwa ampiga risasi mwanamume

Jambazi amvunja shingo ajuza wa miaka 100 kisha kumuibia

adminleo