• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
Akiri alipokea mamilioni kununulia wanakijiji shamba

Akiri alipokea mamilioni kununulia wanakijiji shamba

Na RICHARD MUNGUTI

KINARA wa shirika la kuboresha makao ya wakazi wa vijijini Bi Jane Weru Jumatatu alikiri kuwa alipokea pesa kutoka kwa wakazi 2,200 wa kitongoji cha Mukuru eneo la Embakasi kaunti ya Nairobi kuwanunulia shamba la ekari 23 kwa bei ya Sh81 milioni.

Bi Weru aliyekuwa akitoa ushahidi katika kesi ambapo ameshtakiwa na wakazi hao wa mtaa wa mabanda wa Mukuru alimweleza Jaji Elijah Ombaga.

Mkurugenzi huyo mkuu wa Muungano wa Wanavijiji Akiba Mashinani Trust alimweleza Jaji Ombaga kuwa wakazi hao walimwendea na kumsihi awasaidie kununua shamba hilo la ekari 23 lillokuwa linamilikiwa na kampuni ya Whitemills.

Kinara huyo alisema kuwa kampuni hiyo ilikubali kuuzia wanakijiji hawa shamba hilo kwa bei ya Sh104milioni lakini tukasikizana ipunguze kwa vile hati ya umiliki ilikuwa na kampuni nyingine kwa jina Dhrupa.

Kampuni hii ya Dhrupa ilikuwa imepewa mkopo kununua shamba hilo na benki hiyo ya EcoBank na ikashindwa kuulipa.

“Tulikubaliana na Dhrupa kwamba tutailipia mkopo ndipo hati miliki ya shamba hili liandikishwe kwa jina la Mukuru Makao Bora. Nilikubaliana na Benki hiyo ipatie wanakijiji hao mkopo wa Sh50 milioni ambapo Sh26 milioni italipia mkopo na Sh24 milioni zitawekwa kwa akaunti ya wanakijiji hawa,” alisema Bi Weru.

Alisema wanakijiji walikusanya pesa zikatosha kununua pesa hizo.

“Walalamishi walikusanya pesa na kunipa nikaweka katika akaunti kisha nikalipa mwenye shamba,” alisema Bi Weru.

Wakanakijji hawa waliofika kortini kusikiza kesi dhidi ya Bi Weru wanaomba mahakama kuu imshurutishe Bi Weru awape hatimiliki ya shamba hilo ndipo walistawishe na kujijenga nyumba zao.

Pia wanaomba mahakama kuu imshurutishe Bi Weru awape hesabu ya pesa zilizokatika akaunti yao.

Wanakijiji hawa wanaserma Bi Weru amekawia sana kuwapa hati miliki ya shamba la ilhali walikamilisha kuilipia kitambo zaidi ya miaka 10 iliyoputa.

Akitoa ushahidi  Bi Weru alisema wakati wanakijiji hao walimwuliza awasaidie hawakuwa na pesa za kutosha na walikopeshwa pesa na mashirika mengine ndipo walipe pesa kwa wizara ya ardhi ndipo hatimiliki hiyo ilipiwe pesa za stempu.

Mahakama ilijulishwa pia mkopo huo ulikuwa unapata riba. “Ilibidi niombe benki ya EcoBank iwakopeshe wanakijiji Sh3.5 milioni za kulipa Wizara ya Ardhi.”

Aliongeza kusema kuwa mikopo hiyo ya benki ilikuwa inapata riba.

Mshtakiwa huyo (Weru) aliomba mahakama akubaliwe kuwasilisha ripoti ya mkaguzi wa hesabu kuhusu mkopo huo na wapesa zile alizopokea kutoka kwa wanakijiji hao.

“Naomba mahakama iahirishe kesi ninywe maji. Nahisi kiu. Nimesimama kwa muda mrefu,” Bi Weru alirai.

Jaji Ombaga aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 7 2019 akisema , “Daftari ya kuorodhesha za kusikizwa mwaka huu haina nafasi.”

You can share this post!

Wakili kizimbani kwa kuvunja vikombe na sufuria

Mzee aliyehonga jaji azirai ghafla mahakamani

adminleo