• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 5:55 AM
Majaji na mahakimu walia bajeti ya mahakama kukatwa

Majaji na mahakimu walia bajeti ya mahakama kukatwa

Na RICHARD MUNGUTI

CHAMA cha mahakimu na majaji nchini (KMJA) Jumatatu kiliomba Serikali irekebishe bajeti iliyotengewa idara ya mahakama.

Katika hotuba kwa wanahabari KMJA kupitia kwa katibu mkuu (SG) Bw Derrick Kuto, kilisema hatua ya Bunge la Kitaifa kupunguza bajeti yake ni njia ya kulemaza huduma za mahakama na utekelezaji wa haki.

“Kupunguzwa kwa bejti kutoka Sh31.2bilioni ni njia ya kuvuruga utenda kazi wa idara ya mahakama,” alisema Bw Kuto.

Katibu huyo alisema kuwa hatua hiyo ya bunge ya kupunguza ni njia ya kuendeleza mashambulizi ya idara ya mahakama.

“Kukatwa kwa pesa zilizoombwa na idara ya mahakama ni ishara ya kuendeleza mashambulizi ya kitengo hiki kimoja cha idara ya mahakama,” alisema Bw Kuto.

Alisema idara ya mahakama hutekeleza haki kwa kila Mkenya.

You can share this post!

Raha tele kwa kocha timu yake kuangusha Mathare

Gor yajiandaa kupiga mechi 8 Agosti

adminleo