Na MARGARET MAINA
MTU kuwa na miguu au visigino vilivyopasuka ni dalili tosha kuwa katika mwili kuna upungufu wa virutubisho kadhaa, vitamini au madini.
Hata hivyo, wengi wetu tumekuwa na mitazamo kwamba visigino kupasuka ni ishara tosha kwamba mtu ameonyesha kutojali usafi wa miguu yake.
Kwa kawaida, ngozi zetu huwa zina unyevu ambao huiwezesha ngozi ivutike au kutanuka pamoja na kusinyaa bila ya kutokea madhara yoyote kama vile kuchanika.
Pamoja na ngozi kugawanyika katika sehemu tatu; yaani sehemu ya nje ‘Epidermis’, sehemu ya kati ‘Dermis’ na sehemu ya ndani ‘Endodermis’, ni sehemu ya nje, ambayo ipo karibu na unaweza kuigusa au inaweza kuathirika na ukaiona kirahisi; na hii ni kwa sababu inagusana moja kwa moja na mazingira yetu.
Mitembo huanza kutokea katika sehemu hii ya ngozi, Epidermis.
Miongoni mwa sababu zinazoweza kumfanya mtu apasuke visigino ni pamoja na:
a) Ngozi kuwa kavu sana
Hii ni sehemu ya nje ya ngozi ambayo inawezekana mtu kwa asili yake akawa na ngozi kavu na hivyo kuifanya ishindwe kustahimili kutanuka au kusinyaa na hivyo kusababisha ipasuke.
Kuiacha miguu katika maji kwa muda mrefu na baadaye kutoipaka mafuta ya kulainisha ngozi husababisha ile asili ya ngozi pamoja na mafuta katika ngozi yapotee na kuiacha ngozi ikiwa kavu sana.
b) Kuwa na uzito mkubwa
Hali hii husababisha presha kubwa iwe katika miguu unapokanyaga chini na endapo ngozi yako haitakuwa na uimara wa kutosha itasababisha visigino vipasuke.
Upungufu wa virutubisho mwilini; hasa madini ya Zinc, vitamini E pamoja na mafuta, na Omega 3. Hii husababisha ngozi kupoteza uimara wake na kuifanya ipasuke.
c) Kuvaa viatu ambavyo nyuma vipo wazi
Hulazimisha mguu au upande wa kisigino katika mguu utanuke zaidi na hivyo kuuweka mguu hatarini kupasuka.
d) Magonjwa
Baadhi ya maradhi kama vile Kisukari na magonjwa ya homoni (thyroid diseases) yana athari hasi kwa afya ya ngozi.
e) Umri mkubwa
Kwa kawaida mtu anapokuwa na umri mkubwa sana, hata utendaji kazi wa mifumo mbalimbali katika mwili wake hupungua kiufanisi; hivyo hata kinga ya mwili pamoja na afya ya ngozi pia hupungua.
Mtu kutozingatia usafi wa miguu yake kwa kiwango kinachostahili pia husababisha mipasuko kwenye visigino.
Moja ya madhara yanayoweza kutokea kwa mtu kupasuka visigino ni kupata maambukizi ya magonjwa.
Hii ni endapo miguu itachanika kiwango cha kufikia dermis, kiasi cha kusababisha damu ianze kutoka na kuchangia maumivu makali.
Mtu anaweza kupata maambukizi ya magonjwa kupitia mipasuko hiyo.
Kuzuia au kutibu tatizo la kupasuka visigino
Unafaa: