• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 1:29 PM
Kocha asifu vijana wake kuandaa gozi kama alivyowaagiza

Kocha asifu vijana wake kuandaa gozi kama alivyowaagiza

NA CECIL ODONGO

KOCHA wa Zoo Kericho FC Sammy Okoth amewamiminia  sifa kocho kocho wachezaji wake kwa kusakata gozi kulingana na maagizo yake kwenye ushindi wa 2-1 walioutwaa dhidi ya Kariobangi Sharks katika mechi ya KPL Jumapili Agosti 5 ugani Camp Toyoyo, jijini Nairobi.

Kulingna na mnoaji huyo, kikosi chake kilitumia mbinu za kipekee kuangusha Sharks baada ya kusoma mtindo wao wa uchezaji katika mechi zao za nyuma.

“Kipindi cha kwanza kilikuwa chenye kasi sana  na walituzidi mbio. Hata hivyo tuliweza kudhibiti kasi yao katika kipindi cha pili na wanasoka wangu walitii agizo la kumiliki mpira na kupunguza kasi yao,” akasema Okoth baada ya ushindi huo.

Kocha huyo katika sifa zake hakumsaza mastraika wake ambao walizidisha mashambulizi ya kuvizia langoni mwa wapinzani  huku ushindi huo ukizidi  kuwasongesha mbali  na eneo la hatari la kushushwa daraja.

Hata hivyo mkufunzi huyo alisikitikia hatua ya difenda wake Earnest Kipkoech kulishwa kadi mbili za manjano kisha kutimuliwa kwa kadi nyekundu na akadai kwamba hatua hiyo huenda ikaiponza timu katika mechi zao mbili zijazo.

“Ni pigo kubwa kwetu kwa kuwa Kipkoech alikuwa akicheza katika nafasi ya Nicholas Kipkurui ambaye pia anatumikia marufuku ya mechi mbili. Alikuwa ameimarika sana lakini tuna wingu la matumaini kwamba atakawajibikia nafasi hiyo atang’aa jinsi wawili hao walivyofanya,” akaongeza Okoth.

Baada ya ushindi huo, Zoo Kericho sasa wanashikilia nafasi ya 13 kwenye msimamo wa jedwali la KPL kwa alama 29 baada ya kujibwaga uwanjani mara 25.

Zoo Kericho watakuwa wenyeji wa Nzoia Sugar katika mechi yao ya Agosti 11 itakayogaragazwa Kericho Green Stadium, Kaunti ya Kericho.

You can share this post!

Binti gaidi mwenye umri mdogo zaidi duniani atupwa jela...

Wanandoa wanyweshwa mkojo kwa kuoana kisiri

adminleo