• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 3:04 PM
Google sasa yawezesha watumiaji kutuma baruapepe za siri

Google sasa yawezesha watumiaji kutuma baruapepe za siri

Na BERNARDINE MUTANU

KAMPUNI ya Google imebadilisha mfumo wake wa baruapepe za Gmail, na kuongeza chaguo la kutuma au kupokea ujumbe kwa njia ya siri, na katika hali salama zaidi.

Kulingana na taarifa ya kampuni hiyo,  baruapepe za siri zitafutika baada ya miaka mitano. Pia, aliyetuma ujumbe huo atakuwa na uwezo wa kuufuta ujumbe huo wakati wowote.

Zaidi, wanaopokea jumbe hawatakuwa na uwezo wa kutumia watu wengine, kuzinakili, kuzichapisha au kuzidondoa.

Watumiaji wa Gmail pia wataweza kutengeneza muda wa mwisho wa baruapepe waliyotuma kusalia katika akaunti ya aliyetumiwa. Hii ina maana kuwa baruapepe itajifuta yenyewe baada ya muda huo kukamilika.

Barua pepe kutoka kwa mtumiaji wa Gmail itakuwa ya kawaida, lakini kutoka akaunti nje ya Gmail, kama Yahoo, baruapepe hizo zitakuwa zikifunguliwa nje ya akaunti, katika wavuti salama, imesema Google.

Huenda mtumaji wa baruapepe akawahitaji waliopokea ujumbe kutumia neno siri  kuweza kufungua barua hiyo. Nywila (password) hiyo itatumwa kwa njia ya simu au baruapepe.

Kwa watumiaji wa Gmail, nambari hiyo ya siri itakuwa ikitumwa kupitia kwa simu (ujumbe mfupi). Kwa watumiaji wa akaunti nje ya Gmail, watapokea kodi hiyo kwa baruapepe au kwa ujumbe mfupi.

Lakini watakaopokea kodi hiyo ni wanaoishi Uingereza, India, Japan, Marekani Kaskazini, na Marekani Kusini.

Aidha, unaweza kupiga picha jumbe huo  (screenshot). Ukifungua akaunti yako, ukienda kuandika ujumbe mpya kwa simu au kwa kompyuta, utapokea chaguo (option) la kuandika ujumbe huo kwa namna ya siri (confidential) kwa kutumia nukta tatu upande wa kulia wa skrini ya simu yako, ambapo unaweza kubadilisha usiri wa baruapepe yako.

Kwa kutuma ujumbe kutumia kompyuta, utafungua ‘andika ujumbe’, pale chini kuna kidude mfano wa kufuli. Ikiwa barua hiyo ni ya siri, bonyeza kidude hicho, kitakupa chaguo la jinsi unataka kutuma ujumbe wako.

You can share this post!

IPSOS: Kazi yetu ni kutafiti, si kuhukumu wafisadi

Masaibu ya Sofapaka yaipa Gor ushindi, ubingwa wanukia

adminleo