• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 8:55 AM
EACC yapewa fursa ya mwisho kuwakamata Wakhungu na Waluke

EACC yapewa fursa ya mwisho kuwakamata Wakhungu na Waluke

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA ya kuamua kesi za ufisadi (ACC) Jumatano iliipa Tume ya Kupambana na Ufisadi nchini (EACC) fursa ya mwisho kumkamata Bi Grace Wakhungu anayeshtakiwa pamoja na Mbunge wa Sirisia John Waluke kwa kuilaghai Halmashauri ya Nafaka na Mazao NCPB Sh300 milioni katika kashfa ya mahindi.

Hakimu mwandamizi Bw Lawrence Mugambi alitoa agizo hilo wakati wa kutajwa kwa kesi dhidi ya Bw Waluke.

Mahakama ilifahamishwa kuwa maafisa wa EACC wanaendelea kuweka bidi kumsaka Bi Wakhungu anayekabiliwa na mashtaka ya kutoa ushahidi wa uwongo kwa jopo lililochunguza mzozo kati ya kampuni yao na Bw Waluke iliyodai ilihuifadhia NCPB tani 40,000 za mahindi kwa gharama ya zaidi ya Sh300 milioni

Wameshtakiwa walipokea pesa hizo kwa njia ya udanganyifu. Kesi itatajwa Septemba 25, 2018.

“Ikiwa Bi Walukhe hatakuwa ametiwa nguvuni ifikapo Septemba 25 basi kesi dhidi ya Bw Walukhe itaendelea,” alisema Bw Mugambi.

Hakimu alisem mahakama haitakuwa na budi na kuendelea na kesi dhidi ya mbunge huyo na hatimaye Bi Wakhungu akikamatwa ataadhibiwa kivyake.

You can share this post!

EACC yaagizwa impe Kidero nakala za ushahidi

Kesi ya tatu ya sakata NYS kuanza Februari 2019

adminleo