• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:10 PM
Bei ya sukari kushuka

Bei ya sukari kushuka

Na BERNARDINE MUTANU

Bei ya sukari inatarajiwa kushuka baada ya serikali kuachilia magunia milioni 1.37 ya bidhaa hiyo.

Sukari hiyo ilizuiliwa bandarini kwa kushukiwa kuwa mbaya kwa watumiaji. Mbunge wa Viwanda Peter Munya Jumatano alisema sukari hiyo ilichunguzwa na kupatikana kuwa salama kwa watumiaji.

Wiki iliyopita, wabunge walikataa ripoti ya uchunguzi iliyoonyesha baadhi ya maafisa wa serikali walihusika katika uagizaji wa sukari hiyo kutoka nje ya nchi.

Sukari hiyo imeachiliwa kwa waagizaji wake na inatarajiwa kuongeza kiwango cha sukari nchini, na kupunguza bei ya bidhaa hiyo.

Bei ya sukari nchini imepanda kwa kati ya Sh10 na Sh20 kwa sababu ya upungufu.

“Kwa kuzingatia matokeo ya uchunguzi, serikali itaachilia sukari iliyopatikana kuwa salama,” alisema waziri huyo.

Sukari hiyo itasindikizwa na polisi kutoka bandarini hadi katika viwanda za kuitengenezea ili iuzwe nchini.

You can share this post!

Ruto na Waiguru wachemka kutajwa kuwa wafisadi zaidi

Maafisa wa KEBS kukaguliwa upya

adminleo