Michezo

Arsenal yapewa Bayern Munich hatua ya robo-fainali Uefa

March 15th, 2024 1 min read

NA REUTERS

KLABU ya Arsenal imekutanishwa na miamba Bayern Munich katika droo ya mechi za hatua ya robo-fainali ya Klabu Bingwa Ulaya (Uefa).

Kulingana na droo iliyofanywa Ijumaa, klabu nyingine ya Uingereza, Manchester City–ambao ndio mabingwa watetezi– itakwaana na Real Madrid ya Uhispania.

Nayo Atletico Madrid inatarajiwa kupambana na Borussia Dortmund huku Paris Saint-Germain ikipewa FC Barcelona.