Dondoo

Buda aduwaa kupata mke wake aliyemsamehe kwa kuchepuka ni mjamzito

Na JANET KAVUNGA July 26th, 2024 1 min read

MKAZI mmoja wa hapa amechanganyikiwa baada ya kugundua kuwa mkewe aliyemsamehe kwa kuchepuka, alikuwa na mimba ambayo anashuku sio yake.

Jombi alimfumania mkewe akitoka gesti na buda mmoja na mwanadada akakiri alikuwa akishiriki mpango wa kando na mwanamume huyo na akaahidi kuacha. Jamaa alimsamehe lakini baada ya wiki tatu akagundua demu alikuwa na mimba.

Kwa kuwa alikuwa akichepuka na ufichuzi huo ulijiri muda mfupi baada ya kumsamehe demu, jamaa alichanganyikiwa asijue la kufanya hadi akaanza kulewa kupindukia.

Juzi, alifunguka na kumweleza kaka yake kinachomsumbua na akashauriwa amuulize mkewe mimba ilikuwa ya nani. Lakini alipomuuliza mkewe alichanganyikiwa zaidi alipomuuliza iwapo hakuwa amemsamehe kwa dhati.