Habari Mseto

Diwani akana kuua bila kukusudia

June 6th, 2024 1 min read

NA BRIAN OCHARO

DIWANI wa wadi ya Shimo La Tewa Haron Thethe ameshtakiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia.

Bw Thethe alipofishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Shanzu Bw Robert Mbogo, alikana shtaka la kumpiga mawe hadi kufa Morris Kakunde.

Bw Mbogo aliagiza mshtakiwa kuzuiliwa kwa siku saba.