• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 5:01 PM
Ataka idhini aoe mke wa nduguye

Ataka idhini aoe mke wa nduguye

Na TOBBIE WEKESA

SINOKO, BUNGOMA

Kalameni mmoja kutoka hapa aliwashangaza wengi alipoandaa kikao kuomba idhini ya kumuoa mke wa ndugu yake aliyepotelea mjini kwa miaka mingi.

Inadaiwa polo aliandaa kikao hicho baada ya ndugu yake kupotea kwa boma na kumuacha mkewe akiwa pweke.

Duru zinasema ndugu ya polo hajaonekana kwa boma kwa zaidi ya miaka kumi tangu aondoke kwenda jijini.

Kulingana na mdokezi, polo alidai liandaa hafla hiyo kulingana na mila na desturi za jamii yake.

Inasemekana polo aliwaarifu wazee wa ukoo kuhusiana na mipango yake ya kumuoa mke wa ndugu yake rasmi.

Inadaiwa wazee walipinga mipango ya polo kwani walidai kwamba ndugu yake angali hai.

“Hatujapata habari zozote kuhusu kifo cha ndugu yako. Ni hatia kwako kumuoa mke wake,” mzee wa ukoo alimkashifu polo.

Inasemekana polo hakutaka kumsikiliza yeyote aliyejaribu kupinga mipango yake.

“Huyo jamaa ni kama hana haja na huyu mwanamke. Huyu mke amekaa kwa upweke huku akigongwa na baridi kwa muda mrefu,” polo alidai.

“Wewe tafuta mke wako uoe. Ndugu yako anaweza rudi wakati wowote,” mzee wa ukoo alimkaripia polo.

Polo alisisitiza kwamba mwanamke huyo alikuwa akiumia sana kwa baridi usiku ilhali yeye yuko..

“Huyu ndugu yangu alikuwa ameshapeleka mahari kwao. Mimi sitaki arudi kwao na aolewe kwingine. Ndugu yangu akirudi nitamrejeshea mke wake,” polo alidai huku vicheko vikishamiri.

Wazee walibaki midomo wazi. “Huyu jamaa anasema ukweli. Iwapo mwanamke amekubali kuolewa naye acheni aolewe. Hakuna haja kungoja mtu tusiyejua aliko,” mzee mmoja alisema.

Inadaiwa iliwabidi wazee kuondoka bila kutoa suluhisho.

You can share this post!

Kisasi dhidi ya Amerika ni lazima – Iran

Jinsi kuvuta sigara kiholela kunavyoweza kuingiza mtumiaji...

adminleo