Dondoo

Mke wa pasta achoshwa na tabia ya demu kumkumbatia mume wake eti anajazwa roho

Na KALUME KAZUNGU June 3rd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MTWAPA, Kilifi:

MKE wa pasta mmoja mjini hapa hivi majuzi alimpiga breki demu muumini aliyezoea kumkumbatia mumewe.

Demu huyo amekuwa akidai ni kwa kumpiga pasta pambaja ndipo hujihisi kupokea nguvu mpya za kiroho.

Ni tabia ambayo imemkeketa maini mke wa pasta kwa muda mrefu hadi akaamua kuikomesha.

Punde alipozima jaribio la demu kumfikia pasta hakutosheka, kwani ibada ilipofika tamati alisimama mbele ya kanisa na kutangaza paruwanja kwamba ni mwiko kwa demu yeyote kumpiga pambaja mumewe.

“Wale mademu wanaotafuta roho kwa kumkumbatia bwanangu basi kuanzia leo kaeni bila roho. Sitakubali mchezo huo kwa mume wangu hata kama ni pasta wenu. Huyu ni baba wa watoto wangu. Tuheshimiane,” akafoka mama huyo.