• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Wakazi wakatakata chifu na kuchoma mwili wake

Wakazi wakatakata chifu na kuchoma mwili wake

Alex Njeru na Gerald Bwisa

WAKAZI wenye ghadhabu kutoka kata ya Kamaindi, Kaunti ya Tharaka-Nithi Jumanne walimkatakata chifu wao Japhet Mayau Mukengu vipande vipande kabla ya kumchoma, kufuatia mzozo wa muda mrefu.

Chifu huyo alisemekana kuuawa na wakazi ambao walighadhabishwa na uamuzi wa kakake, Gikware Mukengu, kuzuilia mbuzi wa mkazi kwa jina Gitonga Kibuibe, ambaye alitoweka Desemba mwaka jana, kabla ya mabaki ya maiti yake kupatikana karibu na mto.

Kamishna wa Kaunti hiyo Beverly Opwora alisema kuwa polisi walikuwa wameanzisha uchunguzi kuhusu kisa hicho, ambacho kilishangaza wengi.

“Kulingana na ripoti, chifu huyo aliuawa na wakazi wenye hasira lakini maafisa wetu wanakusanya habari kuthibitisha madai,” akasema Bi Opwora.

Mbuzi hao walisemekana kuwa walikuwa wameingia katika shamba la Bw Mukengu.

Marehemu naye alisemekana kuwa mnamo Desemba 12, 2018 alikuwa ameenda kuoga mtoni lakini hakurudi, wakazi wakidai kuwa aliuawa na wanawe chifu huyo, pamoja na nduguye.

Baada ya kuripoti kisa hicho kwa Naibu Kamishna wa eneo la Igambang’ombe, wakazi wanasemekana kutumwa kwa chifu huyo kuwatatulia kesi yenyewe.

Hata kabla ya chifu kufika, mamia ya wakazi wakiwa na ghadhabu walivamia nyumbani kwa kakake, lakini akafanikiwa kutoroka, naye chifu alipofika wakamvamia kwa hasira, wakimkatakata kwa panga kisha kumteketeza.

Kwingineko, wezi walibomoa ukuta wa jengo la mawe wakitarajia kuiba mali ya thamani katika duka mjini Kitale, lakini wakaishia kupata sarafu za Sh2,000 pekee jana asubuhi.

Wachunguzi waliofika eneo la tukio asubuhi walikisia kuwa huenda wezi hao walitumia saa mbili kubomoa na kutoboa shimo kwenye ukuta, kabla ya kuingia katika duka hilo la Chase Drapers.

 

You can share this post!

Kalonzo ataka sheria kuhusu utajiri wa viongozi ibuniwe

Msanii Chameleone azuiwa kumuona Bobi Wine gerezani

adminleo