• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 12:11 PM
Ajabu ya mazishi kuhudhuriwa na watu 400 katika eneobunge la Mutahi Kagwe

Ajabu ya mazishi kuhudhuriwa na watu 400 katika eneobunge la Mutahi Kagwe

By NICHOLAS KOMU

Serikali imelaumiwa kwa kukosa kuzingatia usawa kuhusu jinsi kanuni zilizowekwa kuzuia kusambaa kwa virusi vya korona zinatekelezwwa.

Hii ni baada ya madai kuibuka kwamba wanasiasa na viongozi hawafuati kanuni hizo, hasa eneobunge la Mukurweini anakotoka waziri wa Afya Mutahi Kagwe, hapo Jumatano ambapo watu 400 waliruhusiwa kuhudhuria mazishi ya mwalimu mtaaafu.

Serikali ilisema kwamba idadi ya watu wanaopaswa kuhudhuria mazishi ni 15.

Lakini katika mazishi haya watu 400 kutoka Kijiji cha Kihate waliruhusiwa kukusanyika katika shule ya msingi ya Mutwewathi kuhudhuria mazishi chini ya ulinzi wa polisi, viongozi na maafisa wakuu wa Wizara ya Afya.

Mkurungezi wa Afya Dkt Patrick Amoth aliiwakilisha Waziri wa Afya Mutahi Kagwe aliyetarajiwa kuhudhuria mazishi hayo.

Mbunge wa Mukurweni Antony Kiai na spika wa kaunti ya Nyeri John Kaguchia walihudhuria. Kikosi cha polisi na maafisa wa kulinda misitu walikuwa kulinda doria.

Wanahabari walizuiliwa kurekodi mazishi hayo na kuamrishwa kufuta video walizorekodi na kufuta picha walizokuwa wamepiga.

You can share this post!

Waendeshaji bodaboda na tuktuk Ganjoni wapewa sanitaiza

Ruto aendea baraka za 2022 kwa wazee

adminleo