• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:10 PM
BOBI WINE: Shinikizo kwa Museveni aachilie huru msanii zazidi

BOBI WINE: Shinikizo kwa Museveni aachilie huru msanii zazidi

Na ANTHONY OMUYA

RAIA wa Uganda wanaoishi Kenya waliandaa maandamano ya amani Agosti 23, 2018  jijini Nairobi kutaka serikali ya Uganda kukoma kumtesa mbunge na mwamamuziki Bobi Wine.

Waandamanaji walianza maandamano kutoka eneo la Freedom Corner kwenye bustani ya Uhuru Park. Zaidi ya watu mia nne waLishiriki kwenye maandamano hayo.

Wakiwa maandamanoni katika barabara ya Kenyatta,  walisema msanii huyo, mwanasiasa maarufu kwa sasa anayefahamika kwa jina halisi  Robert Kyagulanyi, ni mwenye ujasiri mkuu.

Walieleza kwa masikitiko kuwa mataifa mengi hayajachukua hatua za kidiplomasia dhidi ya  rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni wa na kumtaja kuwa dikteta ambaye hastahili kuongoza taifa lolote lenye demokrasia na huru ulimwenguni.

Wandamanaji hao, wakiwemo wanaharakati wa  Kenya, wanamuziki na wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka Kenya na Uganda walishutumu vikali hatua ya serikali ya Uganda na kutaja hatua ya kumshtaki na kumfikisha mahakamani  kama ukiukaji wa  haki za kibinadamu na kuvunja sheria za Umoja wa Kimataifa.

Walitumia vipaza sauti, mabango na nyimbo za msanii huyo za kisiasa  na kutaja kwamba wanapigania uhuru wa nchi ya Uganda, ambayo wanadai imo gizani kwa uongozi wa kiimla.

“Hakuna uhuru Uganda, wakati wa dikteta Museveni kuondoka uongozini umewadia. Yeye na familia yake. Mateke anayorusha ni ya punda. Haya ni mateke ya mwisho,” akasema Joseph Subuga ambaye ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Nairobi.

Aidha wanataka mataifa  yaliyostawi na Umoja wa Kimataifa kuingilia kati na kuiwekea Uganda vikwazo.

“Tunataka Museveni atambue kuwa kamwe yeye  hawezi kuishi bila vikwazo kutoka Umoja wa Kimataifa. Awe tayari kupokea vikwazo kutoka kwa mataifa yaliyostawi. Uganda sio nchi yake bali ya wananchi wengi. Lazima atii sheria,” akafoka mmoja wa waandamanaji, Janet Kisila.

Mwanamuziki huyo na wengine 30  walitiwa nguvuni na wengine wenzake  30  katika mji wa Arua wiki iliyopita kwa madai ya kumiliki silaha. Mashtaka mapya dhidi ya mwanamuziki huyo ni kujaribu kuua bila kukusudia.

You can share this post!

UGANDA: Onyo kwa viongozi dhalimu mapinduzi yaja!

AMANI CAR: Wanamgambo watoa masharti 97 kwa AU

adminleo