• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Gharama za juu za Intaneti nchini Uganda zawafungia wengi nje

Gharama za juu za Intaneti nchini Uganda zawafungia wengi nje

Na MAGDALENE WANJA

IDADI ya wanaotumia mtandao nchini Uganda ilipungua kwa asilimia 30 mwaka 2018 baada ya serikali kuongeza kodi kwenye huduma za simu zinazotumia mtandao.

Serikali ya Uganda iliweka kodi ya asilimia moja kwa shughuli mbalimbali kama vile kutoa na kuweka pesa kwenye simu ambayo iliongeza gharama kutoka asilimia 10 had asilimia 15.

Vilevile, iliongeza kodi mpya kwa zaidi ya huduma 60 za Facebook, WhatsApp na Twitter ambayo ilichangia kuwa Sh200 za Uganda kila siku.

Kulingana na utafiti kuhusu huduma ya Regulatory Treatment of Over the Top Services; kodi ambayo inawekwa bila kuwahusisha wananchi ama kufanya upelelezi kuhusu madhara yake, hali hii imechangia katika watu wengi kuachana na matumizi ya mtandao.

Utafiti huo ulifanywa katika baadhi ya mataifa ya Afrika likiwemo lile la Uganda.

Matokeo ya utafiti huo yalitolewa na kampuni ya Mozilla ikishirikiana na Tume ya Umoja wa Afrika yaani African Union Commission (AUC).

“Hizi ni baadhi ya hatua ambazo serikali inachukua ambazo zinapunguza idadi ya watu wanaotumia mtandao badala ya kuiongeza idadi hiyo,” alisema mshauri wa sera wa Mozilla barani Afrika Bi Alice Munyua.

Watafiti sasa wameshauri nchi za Afrika kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) kukuza uchumi wa nchi.

You can share this post!

Viongozi waelezea umuhimu wa michezo katika utangamano

Mvutano baina ya TSC na Knut washuhudiwa katika kongamano...

adminleo